Sunday, April 28, 2013

CHADEMA KUMSHITAKI MKUU WA MKOA WA ARUSHA MAGESA MULONGO.


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo mkoa wa Arusha(CHADEMA)kimesema kuwakinatarajia kumfungulia mashitaka mkuu wa mkoa wa Arusha MagesaMulongo dhidi ya kauli zake za uchochezi  dhidi ya Chama hicho  lakinipia kauli za vitisho kwa Mbunge Lema ambaye kwa sasa anashikiliwa naPolisi.
Akizungumza na vyombo vya habari mapema jana Katibu wa chama hichoAmani Golugwa alisema kuwa zoezi hilo lipo mbioni kukamilika kwa kuwawanasheria wa chama hicho tayari wameshapewa taarifa hizo
Golugwa alisema kuwa Magesa Mulongo amekuwa kikwazo kikubwa sana kwakuwa sio mara ya kwanza kutoa lugha za uchochezi dhidi ya Chademalakini hata mara nyingine amekuwa akimtuhu Lema kwa uongo uongo haliambayo hadi kwenye mauaji ya chuo cha uasibu ilijitokeza
Aliendele akwa kusema kuwa kama wataweza kupuuzia hali hiyo itazidikuwaumiza sana na ikubambikiwa kesi ambazo si za kwao kama hali ilivyokwa sasa ambapo kuna dalili za Mbunge Lema kubambiwa kesi ya mauajiyaliyotokea katiika chuo cha Uasibu
“tunavyoongea mpaka sasa tayari tumeshawasiliana na wenzetu ambao niwanasheria wa Chadema na tutamfikisha mahakamani huyu Mkuu ili iwefundisho kubwa sana manake kauli zake za uchochezi na za kutupingasisi zinatuchosha sana na mimi kama Katibu naona amefilisika kisera nahata kimawazo kwa kuwa kamwe siwezi mfananisha hata na mtendaji wanguwa chama”aliongeza Golugwa
Akiongelea Kesi inayomkabili Mbunge Lema alisema kuwa mpaka sasamlalamikaji katika kesi hiyo hakuna lakini vitisho alivyotoa mkuu huyowa mkoa vinasema kuwa Lema kwa sasa hatabanduka na wala hatachomokahali ambayo ni fedheha tu lakini wao kupitia kwa mwanasheria waowanajopanga vilivyo kukabiliana na Mkuu huyo wa mkoa
Awali Wakili wa Mbunge Lema ambaye ni Bw Humprey Mtui alisema kuwaanashangazwa na kitendo cha jeshi la polisi kumvunjia hesima mbungeLema na badala yake kumfanya kama Kapurwa mtaani kwa shinikizo lamaslahi ya watu wacheche
Alisema kuwa kwa mujibu wa sheria Lema angepswa kuitwa na Polisilakini kama angetaa basi ndio angeweza kuchukuliwa sheria kama hiyolakini sio kwa kitendo cha polisi walichokifanya cha kuvuka ukuta wanyumba ya mbunge huyo
Bw Mtui alisema kuwa mbali na hayo pia hata haki za msingi kama vilekuswaki na kunywa chai mbunge huyo ananyimwa na Polisi jambo ambalo niukiukaji mkubwa sana wa Sheria ya Maabusu hapa Nchini ukilinganishakuwa yeye bado ni mbunge na tena mwakilishi wa wananchi
Alifafanua kuwa bado watakuwa na mbunge huyo na wataweza kufuatasheria za msingi lakinii kwa wale wote ambao wanamuonea Mbunge huyowatachukuliwa sheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani kwanihali za uoneaji dhdi yake zinaongezeka siku hadi siku.

SUALA LA USAFI WA MOSHI LISICHUKULIWE KISIASA...



round about iliyopo Mjini hapa.ambapo watu mbalimbali wanaodondosha uchafu wanakamatwa na kutozwa faini huku kukuwepo na malalamiko ya kunynyaswa kwa kutozwa shilingi 50,000.

baadhi ya wafanyabisshara wadogo maarufu kama machinga wakiwa wamepanga bidhaa zao chini wakisubiri wateja.
baadhi ya soko lilipo nje ya Kata za katikati ya Mji.


Suala la usafi Moshi lizingatiwe

Rodrick Mushi

MANISPAA ya Moshi ni miongoni mwa manispaa zinazoongoza kwa usafi, lakini hivi sasa suala hilo la usafi wa mazingira linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo ya itikadi za kisiasa.
Kwa upande wa Tanzania, Manispaa ya Moshi ni miongoni mwa manispaa ambazo zimekuwa zikiwavutia wengi, wakiwamo madiwani, wageni mbalimbali kutoka nje na ndani ya nchi kufika na kujifunza jinsi ya kuweka manispaa zao kuwa safi kama Moshi.
Zipo sheria ndogondogo ambazo hutungwa na manispaa ya mji kwa ajili ya kuhakikisha usafi unaendelea kuwapo na watu ambao wamekuwa wakichafua mazingira wanachukuliwa hatua za kisheria pamoja na kutozwa faini.
Kila mgeni anayefika mjini hapa kama ameambatana na mwenzake basi utasikia akimwambia mwenzake, angalia usije ukatupa takataka, ikiwa ni vocha, kichungi cha sigara au kutema mate, kwani utatozwa faini na watu wanaosimamia usafi.
Katika mji huu kuna mawakala wanne ambao ndio waliopewa jukumu la kusimamia usafi wa mazingira, ila kinachonishangaza ni kwamba usafi unaosimamiwa ni Kata ya Kiusa, Kata ya Mawenzi kuzunguka Stendi Kuu, Soko la Kati, Barabara ya Ghala, Barabara ya Mawenzi, maeneo ya Mtaa wa Dar es Salaam, Mawenzi na Posta.
Madiwani wanasema mawakala waliopewa jukumu hilo kwa sasa wamegeuka kuwa magaidi kwani wamekuwa wakiwakamata wananchi na kuwapeleka pasipojulikana na hata wakati mwingine kuwatoza kiasi kikubwa cha pesa kuliko zile zilizowekwa.
Lakini ukweli ni kwamba mawakala waliopewa jukumu la kusimamia usafi wa mazingira wamegeuka miungu watu, kwani hata baada ya baraza kupunguza kiwango cha faini kutoka sh 50,000 hadi sh 10,000 bado waliendelea kutoza kiwango cha sh 50,000 na kudiriki kutoa hata risiti bila woga.
Hivyo kinachochukuliwa na wanasiasa hivi sasa ni kitendo cha baraza la madiwani kuwaondoa mawakala waliokuwa wanasimamia zoezi hilo la usafi wa mazingira na kurudisha manispaa.
Meya wa Manispaa ya Moshi, Japhary Michael, akizungumza kwenye moja ya kikao cha baraza anasema wameamua kuwaondoa mawakala kwa sababu wanawatesa sana wananchi, kibaya zaidi wanawateka wananchi na kuwatoza kiwango kikubwa cha pesa.
Anasema mawakala hao mkataba wao utakwisha Juni 30, lakini hivyo ni vema wakasubiri kwisha kwa mkataba wao ili wasije kuiingiza halmashauri kwenye hasara ya kuwalipa gharama kwa kusitisha mkataba.
Mmoja wa madiwani, Hawa Mushi, anasema kuwa ushahidi upo wa risiti kwa mawakala hao kuwatoza faini kubwa wananchi na kuwapora wananchi mali zao na malalamiko hayo walikwisha kuyafikisha kwa mkurugenzi lakini yanashindwa kufanyiwa kazi kutokana na kampuni hizo za usafi kumilikiwa na  baadhi ya watumishi wa halmashauri.
Kwa mtazamo wangu, ni wakati mwafaka sasa viongozi wa Manispaa ya Moshi kushirikiana kwa pamoja kusimamia usafi wa mazingira ili kuendelea kubakiza heshima ya mji wa Moshi kama ulivyokwisha kujengeka tangu awali badala ya kulaumiana.
Michael anasema kuwa kwa sasa kuna magari yanayozunguka kwenye kata za Manispaa ya Moshi kwa ajili ya kuchukua taka, pamoja na utaratibu uliokwisha kuanzishwa wa madiwani na wenyeviti wa mitaa kufanya usafi kwenye maeneo yao kila mwishoni mwa wiki.
Anasema licha ya jitihada hizo, bado kuna dhana tayari imekwisha kujengeka kuwa mji wa Moshi ni mchafu, na hiyo imetokana na CHADEMA, lengo likiwa ni kuwachonganisha ili wananchi waone kuwa CHADEMA ndiyo chanzo cha mji wao kuwa mchafu.
Kwa mtazamo wangu, lengo la madiwani wa CHADEMA ni kuwanusuru wananchi, kwani tayari kampuni zinazosimamia zoezi hilo zinadaiwa kuwa za vigogo, hivyo ni bora wakatumika askari wa manispaa na mgambo ili amani iendelee kubaki kwa wananchi.

SAKATA LA MACHINGA KUTII KAULI YA MBUNGE MSIGWA , LACHUKUA SURA MPYA IRINGA

polisi Iringa  wakiwa katika  eneo la Mashine tatu ,kuondoa mawe na magogo ambayo yalitumika  kuziba barabara hiyo kama  sehemu ya  kushinikiza  serikali  kuwaruhusu kuendelea  kufanya kazi ya umachinga  eneo hilo  lisiloruhusiwa
Kamati ya  ulinzi na usalama ya wilaya ya Iringa ikiwa  imekutana mchana  huu kwa  kikao cha dharula  kufuatia Machinga  kutekeleza kauli ya mbunge Msigwa  ya kuvunja sheria
Hii  ndio hali halisi  iliyopo  eneo la mashine tatu baada ya machinga  kurejea  eneo hilo leo



KAULI mbunge wa jimbo hilo Mchungaji Peter Msigwa (Chadema) kuwataka wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) kurejea kufanya kazi katika eneo la barabara ya Mashine tatu
nusuru asababishe machafuko makubwa eneo hilo kati ya  polisi na Machinga.
 
Msigwa ambae aliitoa kauli hiyo mwanzoni mwa  wiki  iliyopita  katika mkutano wa wabunge wa chadema waliosimamishwa bungeni ,mkutano uliofanyika katika uwanja wa Mwembetogwa mjini hapa,kwa kuwataka Machinga kurejea eneo hilo na iwapo mtu atafika kuwanyanyasa basi wana----!!!?
Machinga hao jana wameitikia kauli hiyo kwa kurejea eneo hilo na kupelekea askari wa kutuliza ghasia (FFU) kutanda eneo hilo na kushindwa kutumia nguvu zaidi ya kuwataka wafanyabiashara hao kuendelea na shughuli zao eneo hilo .
Wakizungumza na mwandishi  wa habari hizi eneo la tukio  wafanyabiashara hao  walisema  kuwa  wamelazimika  kurejea  katika  eneo  hilo baada ya mbunge  wao Mchungaji Msigwa  kuwaruhusu  kufanya biashara katika  eneo hilo ambalo mwanzoni  walihamishwa na kupelekwa Mlandege .
Hivyo  walisema  ilikuwa ni  vigumu kwao kuondolewa na  polisi katika  eneo hilo ambalo mbunge kama mwakilishi  wao bungeni na vikao  vya baraza la madiwani amewaruhusu .
“ujue  tulianza  kuwashangaa sana polisi wa FFU kufika katika  eneo hili na mabomu ya machozi kutaka kutotoa  wakati wao wenyewe  walikuwepo katika mkutano  wa Chadema pale mwembetogwa ambapo mbunge wetu Msigwa alituruhusu kurejea  eneo hili….kweli  tungeshindwa kulielewa jeshi la  polisi iwapo  wangetumia nguvu kutuondoa  sisi  wakati aliyetoa kauli ya  kuturuhusu anafahamika “
 
Kwa  upande  wake mwanasheria  wa Halmashauri  ya Manispaa ya Iringa, Innocent Kihaga alisema  kuwa eneo hilo kisheria limepigwa marufuku kwa  biashara  za umachinga na  kuwa kwa mtu ambae atapatikana akifanya biashara hapo faini yake ni shilingi 50,000 ama kifungo cha miezi sita jela ama vyote kwa pamoja.
Hatua  hiyo ya machinga  kurejea  katika  eneo hilo la barabara imeonyesha  kuichanganya  serikali ya  mkoa  wa Iringa na  kulazimika  kukutana kwa masaa kadhaa na kamati ya  ulinzi na usalama.
 
Akizungumzia suala  hilo mwenyekiti  wa kamati ya  ulinzi na usalama ya wilaya ya Iringa na kaimu mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Dr Leticia Warioba ambae ni mkuu  wa wilaya ya Iringa  alisema  kuwa serikali  ya mkoa  inapinga kwa  nguvu zote kitendo cha wafanyabiashara hao kurejea  eneo hilo.
Dr Warioba alisema  kuwa anashangazwa na hatua ya  mbunge  Msigwa  kuwaruhusu  wafanyabiashara hao  kuvunja sheria  wakati mbunge  huyo katika  vikao  vya baraza la madiwani katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ni diwani ni katika maamuzi ya  kuwatoa wafanyabiashara  hao alishiriki .
 
Hata  hivyo Dr Warioba  aliwataka wafanyabiashara  hao kwa  jumapili  ijayo  kutofanyabiashara  eneo hilo na kuonya  wale  wote watakaokiuka kauli  hiyo na sheria iliyowekwa  juu ya kutofanya biashara  katika maeneo yasiyo rasmi.
Wakati huo mbunge wa jimbo la Mbeya mjini ,Joseph Mbilinyi (MR SUGU) jana  ameonekana katika Manispaa ya Iringa akiingia katika mashine ya kutoa pesa ATM ya NMB iliyopo nje ya jengo hilo la Manispaa ya Iringa na kusalimiana na viongozi wa Manispaa waliokuwepo nje ya jengo hilo.
BREAKING NEWS...IRINGA SI SHWARI MVUTANO KATI YA MACHINGA NA POLISI WATISHIA USALAMA

Machinga wakiendelea na  shughuli zao kama kawaida  eneo la mashine  Tatu asubuhi  hii kutokana na kauli  ya mbunge Msigwa kuwaruhusu kurejea ,chini polisi  wakiwa eneo hilo

Hali  si  shwari katika Manispaa ya Iringa baada ya kauli   mbunge  wa  jimbo hilo Mchungaji Peter Msigwa (Chadema) kuwataka wafanyabiashara  wadogop wadogo (machinga) kurejea kufanya kazi katika eneo la barabara  ya Mashine  tatu kutekelezwa na machinga  hao.
Msigwa ambae  aliitoa kauli hiyo April 23 mwaka  huu katika mkutano wa wabunge wa chadema  waliosimamishwa  bungeni ,mkutano  uliofanyika katika  uwanja  wa Mwembetogwa  mjini hapa,kwa  kuwataka Machinga  kurejea  eneo hilo na iwapo mtu atafika  kuwanyanyasa  basi wana----!!!?
Machinga  hao  leo  wameitikia kauli  hiyo kwa  kurejea  eneo hilo na kupelekea askari  wa  kutuliza ghasia (FFU) kutanda  eneo hilo na kushindwa  kutumia nguvu  zaidi ya  kuwataka wafanyaiashara hao  kuendelea na shughuli  zao  eneo hilo .
habari na francis godwin.Iringa.

.
 Timu ya waandishi wa habari ya mpira wa pete(waliovalia jezi za rangi ya njano)wakiwa na wachezajiw a Marenga Investment.

 Katika mtanange huo timu ya Waandishi wa habari iliweza kuibuka kidedea kwa kuwafunga Marenga mabao 35 kwa mabao 12 hadi mwisho wa pambano.



        KWA UPANDE WA MPIRA WA MIGUU MAMBO NAYO YALIKUWA HIVI
           WAANDISHI WA HABARI 5-MARENGA 3 HADI DAKIKA 90.
Mchezo huo wa kirafiki ulirushwa moja kwa moja na radio moshi fm ambapo waandishi wa habari walianza kupata bao lao la kwanza dakika ya 1 ambapo hadi kipindi cha kwanza kinamalizika waandishi waliokuwa wakiongoza kwa bao 3.

Hadi mwisho wa mpira waandishi waliongoza timu zote za mpira wa miguu na mpira wa pete hivyo kuweka historia mpya katika uwanja wa mpira wa Chuo Kikuu cha Ushirika(MUCOBS) Mjini Moshi.

 Hapa ni timu ya waandishi wa habari wakingozwa na james Paul wa kwanza kushoto wakijiandaa kuingia uwanjani wakiwa wamevalia jezi nyekundu kama za Man United.
 Timu ya Marenga wauza unga hawa waliweza kulambishwa unga na Sukari hatimaye kumwaga chozi uwanjani.


Thursday, April 18, 2013

MEYA WA MOSHI "HATA BODA BODA NI USAFIRI KAMA USAFIRI MWINGINE..

 Meya wa Moshi,Japhary Michael (Chadema)kama alivyokutwa na kamera ya Tanzania leo akitumia usafiri wa bodaboda kama mwananchi wa kawaidai licha ya kuwa na gari la Meya pamoja na yeye mwenyewe kumiliki magari.

KITIMA "DEMOKRASIA YA TANZANIA IMETEKWA NA WATU WACHACHE"

Makamu mkuu wa chuo Kikuu cha St Augustine Dr Charles Kitima Akisisitiza jambo wakati akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari,hawapo pichani.




Na Rodrick Mushi,Mwanza.

, amesema kuwa demokrasia ya Tanzania imetekwa na watu wachache,huku kukiwepo na msukumo mkubwa kutoka chama tawal (CCM),kuendelea kukandamiza demokrasia ya vyama vingi ili kiendelee kubaki madarakani.

Kitima aliyasema hayo mwishoni mwa wiki, wakati akifunga mafunzo kwa waandishi wa habari za uchunguzi za biashara kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini yaliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Best Ac, jukwaa la kilomo(ANSAF)kwa kushirikiana na  chuo kikuu cha St Augustino Mwanza.

Mbali na kuwepo kwa matukio mbalimbali ya ukandamizaji wa demokrasia  Kitima alisema kuwa muda wa CCM kuondoka madarakani ukifika wataondoka kwa aibu na wataingiza taifa kwenye mahafa mabaya mbeleni.

“CCM ni chama kizuri na sera zake ni nzuri ila kinaponzwa na watu wachache, mwisho wa siku wananchi wataikataa kwa kutoleta mabadiliko pamoja na kutotaka kuondoka madrakani”Alisema Kitima.

Alisema kuwa nchi ya Tanzania ingepaswa kuongozwa kwa nchi za afrika mashariki kuwa nchi yenye demokrasia bora,kutokana na misingi aliyoacha baba wa Taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere lakini misingi hiyo imepotoshwa na baadhi ya viongozi waliokosa uadilifu.

Kitima anasema  kuwa demokrasia ni kujali utu na kuheshimu haki ya kila mtu,watu kujitawala na kuweka serikali inayowajibika kwao,na pindi itakashindwa kuwajibika itapaswa iondoke na kuomba msamaha kwa kushindwa kuwatendea haki wanananchi walioichagua.

“Inasikitisha nchi yenye demokrasia na mfumo wa vyama vingi kusikia chama tawala kikijidai majukwaani kuwa kitaendelea kutawala milele,wakati wananchi ndiyo wenye maamuzi ya mwisho,huo unaweza ukawa ni ukiukwaji wa demokrasia au kujiendesha kidikteta”Alisema Kitima.

Kutokana na matukio ya kutekwa kwa demokrasia Kitima alisema kuwa hali hiyo inaendelea kulelewa nchini,na kuendelea kukua kwani mtu ambaye anaweza kuiba kura kwenye uchaguzi au kugaramikia wizi wa kura anapewa cheo na kudhaminiwa.

Matukio mengine ya ukiukwaji wa demokrasia aliyoelezea Kitima ni pamoja na kufunguliwa kwa kesi wabunge wa upinzani zaidi ya 10 kwa wakati mmoja,na kushinda kuwatumikia wananchi,huku akihoji ni kwa nini hakuna Mbunge wa chama tawala ambaye amekuwa akifunguliwa kesi kama wanavyofanyiwa wa upinzani?

Hata hivyo alieleza kuwa kwa nchi yenye Demokrasia wananchi wanapaswa kua na sheria zao,ikiwa ni pamoja na haki ya kuwawajibisha viongozi waliowachagua kwa kushindwa kuwajibika kwao.

Alisema kuwa Mwalimu Nyerere alijenga misingi mizuri ya demokrasia nchini ya watu kuheshimiana na kuheshimu haki za wengine,lakini misingi hiyo imeachwa na baadhi ya viongozi wa sasa.

“Wakati wa enzi za Mwalimu Nyerere michezo hiyo haikuwepo na alikuwa akigundua unataka kuteka demokrasia kwa kuwanyima haki wananchi usingeweza kupata madaraka kama inavyofanyika hivi sasa”Alisema Kitima.

Mwisho

MATAJIRI WAMIMINIKO KUMUAGA BILIONEA WA MOSHI BABU SAMBEKE.

 




DSCF8840
DSCF8833
MWLI WA bobu sambekeDSCF8828
DSCF8830 DSCF8844    

PICHA ZA SAFARI YA MWISHO YA BI KIDUDE...


Picha za mazishi ya Bi. Kidude. Viongozi wa serikali kama rais Jakaya Kikwete, rais wa Zanzibar Ali sheni, makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar maalim Seif Sharif Hamad, na wasanii kama Mzee Yusuf, Diamond Platnumz, nk walikua miongoni mwa wahudhuriaji katika kumsindikiza gwiji huyo wa Taarabu katika safari yake ya mwisho.

Tuesday, April 9, 2013

Profesa Lipumba, alia na uchumi wa Tanga




Profesa Lipumba, akiiangalia ukuta uliojengwa na wananchi wa Kijiji cha Kigombe mkoani Tanga, mara baada ya kuuzindiwa, kushoto ni Mwenyekiti wa Kijiji hicho Mzee Said.
 Mwenyekiti wa Kijiji cha Kigombe Mzee Said, akitoa maelezo kwa Profesa Lipumba kuhusu ujenzi  wa kingo ya Bahari ambao umejengwa kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa thamani ya Sh milioni 108.



Profesa Lipumba, akiiangalia ukuta uliojengwa na wananchi wa Kijiji cha Kigombe mkoani Tanga, mara baada ya kuuzindiwa, kushoto ni Mwenyekiti wa Kijiji hicho Mzee Said.
 Mwenyekiti wa Kijiji cha Kigombe Mzee Said, akitoa maelezo kwa Profesa Lipumba kuhusu ujenzi  wa kingo ya Bahari ambao umejengwa kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa thamani ya Sh milioni 108.





 washiriki wa kongamano hilo wakimsikiliza kwa makini. 3. Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Tanga Amina Mwidau (CUF), akifuatilia mada kuhusu uchumi wa mkoa  inayowasilishwa na Profesa Lipumba.

Profesa Lipumba, akipata maelezo ya zahanati ya Kijiji cha Kigombe kutoka kwa Daktari wa zahanati hiyo Dk. Uwesu Mtulia.



Na Mwandishi Wetu, Tanga
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba amesema Mkoa wa Tanga ni moja kati ya mikoa maarufu kwa viwanda nchini lakini hivi saa hali ya kimaendeleo katika mkoa huo imekuwa mbaya.
Kauli hiyo ameitoa leo mjini hapa alipokuwa akiwasilisha mada inayohusu maendeleo ya uchumi kwa Mkoa wa Tanga katika kongamano lililoandaliwa na Chama cha Wananchi (CUF) kwa kushirikiana Taasisi ya Maendeleo ya demokrasi kwa vyama vya siasa ya nchini Denmark (DIPD).

Profesa Lipumba alisema kuwa  hakuna haki bila kuwa na maendeleo yanamgusa mwananchi wa kawaida.

Alisema Mkoa wa Tanga imefanikiwa kuwa na rasimali nyingi ikiwemo zao la Mkonge ambalo kwa sasa limekosa msukomo hali inayochangia umaskini kwa wananchi wa mkoa huo.

"Pamoja na Tanga kuwa na fursa nyingi za kiuchumi lakini bado kadri siku zinavyokwenda umaskini umekuwa ukiwatesa wananchi. Viwanda vilikuwa zaidi ya 70 lakini sasa hakuna hata kimoja kinachofanya kazi huku zao la mkonge lilikosa msukumo wa makusudi kwa wananchi wake.

"Katika soko la dunia inaonyesha kuwa Tanga ilikuwa ikizalisha tani 234,000 kwa mwaka lakini sasa mkonge umeporomoka na kufikia tani 25,000 tu hali ambayo imekuwa ikiongeza umaskini kila kukicha. Kama kungekuwa na msukumo wa makusudi wa kufufu zao hili ni wazi Tanga ingekuwa imepaa kimaendelo kwa wananchi wake kutokana na kuwa na kila aina ya rasilimali zikiwemo za matunda na mbogamboga," alisema Profesa Lipumba

Profesa Lipumba, ambaye ni mtaalamu wa masuala ya uchumi duniani, alisema ili kuweza kufikia malengo ya mkoa huo kuweza kupambana na umaskini ni lazima serikali ikubali kwa kufanya uwekezaji hasa katika kufungua bandari ya Tanga ambayo ni lango kuu la kiuchumi.

Alisema Bandari ya Tanga imekuwa haitumiki ipasavyo hali inawechangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa umaskini na hazorotesha harakati za mkoa na wananchi kwa ujumla.

"Bandari ya Tanga, zao la mkonge pamoja na kukosekana kwa msukumo wa kuimarisha sekta ya elimu ni moja ya masuala yanayoufanya mkoa huu kuzidi kurudi nyuma kiuchumi pamoja na wananchi wake,” alisema Profesa Lipumba.




Monday, April 8, 2013

KIKULETWA KUFUFULIWA JE CHUO CHA ARUSHA KITAWEZA KUZALISHA UMEME KAMA ILIVYOKUWA APO AWALI??


Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama(Katikati) akipata maelezo ya Kituo cha Kuzalisha umeme cha Kikuletwa kilichopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro kutoka kwa Mtaalamu wa Chuo cha Ufundi Arusha,Aliyesimama nyuma ya mkuu wa mkoa mwenye miwani ni mkuu wa chuo hicho Dk Richard Masika


Chuo cha Ufundi Arusha kimeanza mkakati wa kufufua mitambo ya kuzalishia umeme wa maji wa Kituo cha Kikuletwa iliyopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro ambapo hadi itakapokamilika itaweza kutosheleza mahitaji ya mikoa ya Kilimanjaro na Arusha na umeme mwingine kubaki.

Ufafanuzi huo umetolewa na  mkuu wa Chuo hicho Dk Richard Masika kwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama aliyetembelea mitambo hiyo ambayo imekabidhiwa kwa chuo hicho na Shirika la Umeme Nchini(TANESCO)

Alisema kuwa chuo hicho ambach kitakuwa cha kwanza barani Afrika kumiliki kituo cha kufua umeme,kitatumia kituo hicho kwa malengo matatu ambayo ameyataja kuwa ni pamoja na kutumika kwa mafunzo,kutengeneza vipuri vya mitambo ya umeme pamoja na kuzalisha umeme.

Dk Masika ameeleza kuwa baada ya kukabidhiwa kituo hicho mapema wiki iliyopita na baadaye kuanza kazi za awali wamebaini kwamba kwa kufunga mitambo mipya ya kufua umeme wataweza kutoa megawati 17 ambazo zitaingizwa katika gridi ya taifa.

“Kiasi hicho kitaweza kutosheleza mahitaji ya umeme kwa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha na kiasi kingine kubaki,”

Akifafanua zaidi alisema kuwa kituo hicho ambacho kilijengwa mwaka 1930 kwa sasa kina mashine tatu ambazo zilikufa na kuacha kuzalisha umeme mwishoni mwa miaka ya Themanini zikiwa na uwezo wa kuzalisha umeme kati ya megawati moja na moja na nusu.

Dk Masika ameeleza kuwa mashine mbili kati ya hizo tatu chuo chake kina uwezo wa kuzifufua na kuanza kufua umeme utakaoingizwa katika gridi ya taifa wakati chuo chake kikiendelea na mkakati wa mpango mkubwa wa uzalishaji umeme kwa kutumia mitambo ya kisasa

Kwa upande wa mafunzo,Dk Masika ameeleza kuwa cuo hicho kimelenga kutoa idadi kubwa ya wataalamu wafanyakazi ambao wenye taalamu ya stashahada ambao kwa kawaida ndiyo wacahapa kazi ili kuzipa pengo la sasa la idadi kubwa kukimbilia katika shahada na baada ya kuhitimu kwa wasimamizi na si wachapa kazi

Alisema kuwa mitambo ya kituo hicho chenye eneo la jumla ya Ekari 400 yanategemea maji ya mito miwili ambayo Kware unaoanzia Mlima Kilimanjaro na Mto Mbuguni unaonzia mlima Meru ambapo maji hayo huduma katika kipindi kizima cha mwaka na kuongezeka wakati wa kiangazi

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Kilimanajro,Gama amewataka wataalamu wa cuo hicho pamoja na mipango mizuri na kuonyesha kuwa na uwezo mkubwa wa kukiendesha lakini aliwataka kuwa na uzalendo ambao utalisaidia taifa katika kutatua tatizo la upatikanaji wa nishati ya umeme.

Alisema kuwa ni vyema sasa wakatambua kwamba taifa limewapa dhamana kubwa kwa kuwakabidhi raslimali kubwa ambayo inatakiwa kusimamiwa vyema kwa ajili ya manufaa ya watanzania na siyo ya watu binafsi.

Gama aliwataka kuhakikisha wanatunza vyanzo vya maji yanayotumika katika mitambo hiyo vya Chemka kilichopo wilayani Hai na cha Mto Mbuguni ambacho kipo wilayani Arumeru mkoani Arusha.

Alisema kuwa uongozi wa serikali mkoani Kilimanjaro unakiweka kituo hicho katika miradi yake mikubwa ya kimkoa na utakuwa tayari kikusaidia chuo hicho wakati wowote kitakapohitaji msaada wa hali na mali.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga ameahidi kukipa ushirikiano chuo hicho na kukitaka kuhakikisha kinaimarisha kitengo chake cha uhusiano ili kujenga mahusiano na vijiji vinavyozunguka kituo hicho.

Alisema kuwa kutokana na mazingira yanayozunguka kituo hicho kutunzwa vizuri katika miaka yote tangu uzalishaji uliposiamama,mara nyingine wakati wa ukame mkali baadhi ya wenyeji ujaribu kuingiza mifugo kwa ajili ya kupata malisho na hivyo kusababisha vurugu.

Makunga alisema kuwa ni vyema chuo hicho kikajipanga kwa kushirikiana na uongozi wa wilaya katika kuhakikisha kinawaelimisha wananchi wanaoishi maeneo ya jirani ili watambue umuhimu wa kituo hicho na madhara ya kutaka kuingiza mifugo kwa nguvu

Tuesday, April 2, 2013

WAANDISHI WA HABARI ZA UCHUNGUZI ZA BIASHARA NA UCHUMI IBJ WAANZA MAFUNZO YAO ST AGOSTINO UNIVERSITY MWANZA...

Kaimu Mkuu wa Chuo kikuu cha St Agustiono Mwanza Padre Tadeus Mkamwa akizungumza na waandishi wa habari wanaosoma mafunzo ya uandishi wa habari za uchunguzi za biashara course ambayo ilianza mwaka jana

Mkufunzi wa chuo kikuu cha St Agustino Denis Mpagaze akitoa mada kwa waandishi wa habari(hawapo pichani).

Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini,television,magazeti na radio,ambao ni wanafunzi wa course ya habari za uchunguzi za biashara yanayoendelea chuo Kikuu  cha St Agostino Mwanza.
WAANDISHI wa habari nchini wamesisitizwa kusoma zaidi ili kuboresha taaluma zao kwa lengo la kuisaidia nchi kutokana na matatizo yanayoikabili.

Makamu mkuu wa chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino(SAUT)Dk,Padri Thadeus Mukamwa amewaambia waandishi wa habari 16 wanaosoma kozi za uandishi wa habari za uchunguzi  biashara katika chuo kikuu hicho.

Amesema waandishi ni chachu ya mabadiliko hivyo wanapaswa kujiongezea maarifa ,”tumieni maarifa hayo kwa maslahi ya umma wala si kwa maslahi yenu….angalieni maslahi ya umma kwanza”alisema.
Alitoa mfano wa nchi ya Marekani kuwa wagombea wake walitanguliza zaidi nchi kuliko nafasi zao.

“Uhuru wa waandishi katika nchi zingine unalindwa sana …ingawa kwetu hapa kuna matatizo mengi yanayowasibu…lakini jikiteni zaidi kuandika ukweli kwa kuibua changamoto zinazokabili jamii”alisema Mukamwa.

Mmoja wa wakufunzi wa kozi hiyo iliyoanza julai 2012 chini ya ufadhili wa Best –Ac,Ansaf na Saut aliwataka waandishi kuwa na malengo ili kuboresha taaluma yao.
“Someni,fanyeni utafiti ili msiwe waandishi wa kupelekwa na wimbi la wanasiasa …chambueni issue ili muweze kuleta mabadiliko kwa kuibua mambo ambayo yanatasaidia kukuza uchumi wa nchi na kufichua mambo yanayosumbua kama mikataba “alisema.