WANANCHI WACHANGA SHILINGI MILLION 12 KWA AJILI YA UKARABATI WA BARABARA AMBAO HAIJAWAHI KUJENGWA TANGU UHURU..
Wananchi wa Kijiji ch mahime Kata ya Old Moshi Mashariki wakitandaza moramu kwenye barabara inayotoka kiboroloni hadi old moshi kidia baada ya kutopitika kwa muda mrefu hususani kipindi cha masika. |
Wananchi wa Kijiji cha Mahome Kata ya Old Moshi Mashariki
wamechoshwa na ahadi ambazo wamekuwa wakiahidi viongozi akiwemo Mbunge wa Jimbo
hilo Cyril Chami na kuamua kuchanga fedha zao mfukoni zaidi ya Shilingi million
12 kwa ajili ya ukarabati wa barabara yenye urefu wa kilometa 4.7 ambayo
imekuwa haipitiki kwa muda mrefu.
Wakizungumza na waandishi wa habari wakiwa kwenye zoezi la
ukarabati wa barabara hiyo inayotoka eneo la kiboroloni kuelekea Old Moshi Kidia imekuwa haipitiki kwa muda mrefu lakini pia imekuwa ikisababisha vifo vya
akina mama na wagonjwa pamoja na wagonjwa wenye hali mbaya kwa kushidnwa
kufikishwa hospitali kubwa kwa wakati.
Mmoja wa wananchi wa Fatael Ulomo kutoka kwenye kijiji hicho alisema
kuwa wakina mama wajawazito wamekuwa wakipoteza maisha hususani wakati wa masika,licha ya
kuwepo kwa shughuli mbalimbali za kimaendeleo kwenye kata hiyo na taasisis zaidi ya tano zinazotegemea
barababara hiyo.
Regnald Maro ambye ni mwenyekiti wa Mtaa alisema kuwa
wananchi waliamua kuchaganga zaidi ya shilingi 10,000 kila mmoja na wengine
kutoa hadi 300,000 baada ya kuachoshwa
na ahadi za uongo kutoka kwa viongozi mbalimbali hivyo kuamua kuachana na siasa na kutumia feha
zao wenyewe.
Kwa upande wa diwani wa Kata ya Old Moshi Mashariki
Aunwilfred Ringo alisema kuwa wananchi wa Kata hiyo wameamua kujitokeza kwa
kujitolea fedha zao pamoja na nguvu zao baada ya kuchoshwa na ahadi za viongozi
wanaowachagua pamoja na Serikali kuahidi bila kuwepo na mafanikio kwenye
ukarabati wa barabara hiyo.
Ringo alisema kuwa licha ya wananchi kuchanga kiasi hicho cha
fedha lakini wana zaidi ya jumapili 12 wakijitokeza barabarani kwa ajili ya
kuusambaza moramu ambao umemwagiwa barabarani ili kuweza kufanya shughuli zao
za maendeleo pamoja na kuwaponywa wagonjwa ambao wamekuwa wakifariki kutokana
na barabara hiyo kuwatopitika.
Hata hivyo Ringo alisema kuwa barabara hiyo haijawahi
kutengewa fedha na halmashauri licha ya kuwa chini ya Halmashauri ya Moshi
Vijijini,ambapo alibanisha kuwa kwenye bajeti iliyopitishwa na 2011/12 barabara
hiyo imeombewa million 65 kwa ajili ya ukarabati wake.
Mwisho
No comments:
Post a Comment