Tuesday, July 31, 2012

MAKUMBUSHO YA BUJORA,MOJA YA VIVUTI VILIVYOSAHAULIKA LICHA YA KUTOA FURSA YA AJIRA KWA WASANII.
Charles Madatta,kwa niaba ya Fabian Mhoja ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Makumbusho hayo akionyesha nyumba walizokuwa wakiishi enzi hizo,na wasukuma.


Moja ya nyumba ambazo zilikuwa zikitumia na wafalme wa Kisukuma kwa ajili ya kukutana na kucheza ngoma za asili ya  kisukuma.



Makumbusho ya tamaduni za kabila la kisukuma yaliyopo Kijiji cha Kisesa Jijini Mwanza yameelezwa kuendelea kuwa kivutuo kikubwa afrika Mashariki na kuwavutia watalii kutoka nchi mbalimbali za jumuiya ya Ulayana  kuchangia katika kuliingizia taifa fedha za kigeni.

Akizungumza na blog hii,Charles Madatta,kwa niaba ya Fabian Mhoja ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji  wa Makumbusho hayo alisema kuwa uwepo wa makumbusho hayo,licha ya kusaidia kutunza mila za kisukuma,lakini pia yametoa ajira kwa wananchi wanaozunguka makumbusho.

Alisema kuwa makumbusho hayo yametoa ajira kwa zaidi ya watu 100  kwenye idara mbalimbali, Miongoni mwa ajira inayotolewa na bujora ni pamoja na wasanii wa ngoma za asili ya kisukuma  kujipatia kipato kupitia sanaa yao,kwa kualikwa ndani na nje ya nchi kama Dernmark,Marekani,Ufaransa.
Alisema kuwa vipo vikundi vya ngoma zaidi ya 2000 ambavyo hualikwa kwa ajili ya kufanya maonyesho ya ngoma hizo,ambapo kwa mwaka vikundi zaidi ya 30 huweza kwenda nje ya nchi,na kutoa mchango wa kodi pamoja na wao wenyewe kunufaika na safari hizo.
Jamii inayozunguka makumbusho ya Bujora wanasema kuwa makumbosho hayo yameweza kuwa mkombozi mkubwa hususani wajasiriamali wadogo wadogo,wakiwemo mama ntilie,dereva wa bodaboda na wananchi wengine ambao hupata nafasi ya kufanya kazi kama nlivyokwishaeleza hapo awali
.
Hata hivyo kwa upande wa vikundi ambavyo vinacheza ngoma za kisukuma vimekuwa vikilipwa zaidi ya 150,000 hadi 200,000 pamoja na usafiri wanapoalikwa kutumbuiza sehemu mbalimbali za Jiji la Mwanza.
Miongoni mwa makumbusho Makumbusho nayopatikana bujora ni pamoja na historia ya kabila la kisukuma,picha ambazo zinaonyesha matukio ya asili,bidhaa za kazi za mikono, historia ya uchifu, uhusiano wa kijamii, teknolojia ya uhunzi, sayansi ya uganga wa kijadi na mifumo ya kuhesabu na majina ambayo yanafuata mfumo wa kijinsia na umri wa watu wanaohesabu namba.



No comments:

Post a Comment