Sunday, March 25, 2012

ZOEZI LA MANISPAA YA MOSHI KUWA KATIKA HADHI YA JIJI,KUKAMILIKA MWISHONI MWA MWAKA HUU..Mmiji wa Moshi Unavyoonekana hivi sasa,Jengo la Kibo Tower




Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Bernadette Kinabo akizungumzia zoezi la Mji wa Moshi Kuwa katika hadhi ya jiji.

Zoezi la upanuzi wa Manispaa ya Moshi kuwa katika hadhi ya jiji linatarajiwa kumalizika mapema mwishoni mwa mwakaa huu baada ya hatua za awali kumalizika.

 Hatua hizo za awali ambazo zimekamilika hadi sasa ni pamoja na upanuzi wa kilomita za mraba 142 tofauti na kilomita za awali ambazo zilikuwa kilomita za mraba 58.

Akizungumza na dira ya leo ofisini kwake Mkurugenzi wa Manisoaa ya Moshi Bernadette Kinabo amesema kilomita za ziada zimepatikana kutoka halmashauri ya Moshi Vijijini jambo ambalo hapo awali liliwekewa urasimu na viongozi waliomaliza muda wake akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo.

Kinabo amesema kuwa zoezi hilo  huenda likakamilika mwishoini mwa mwaka huu,baada ya kupitishwa kwenye halmashauri ambazo mji utapanukia,pamoja na usshirikiano Mkubwa aliouonyesha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama.


Amesema kuwa hali imekuwa nzuri katika mchakato huo baada ya uongozi wa halmashauri ya moshi vijijini kubadilika,kutokana na aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kuzuia wananchi kukubaliana na suala hilo ambalo lilikuwa na maslahi kwa wananchi na ardhi yao ingepanda dhamani badala ya kutegemea kilomo pekee.





No comments:

Post a Comment