MBUNGE WA
HAI NA MWENYEKITI WA CHADEMA TAIFA FREEMAN MBOWE AKIWA KWENYE HARAMBEE
YA UNUNUZI WA GARI LA KUTOLEA HUDUMA ZA NENO NA MUNGU KANISA LA KKKT
USHARIKA WA SIHA MKOANI KILIMANJARO
Mbunge
wa jimbo la Hai Freeman Mbowe amechanga kiasi cha
shilingi million 10 kwenye harambe iliyofanyika kwenye kanisa la Kiinjili la
Kilutheri Tanznaia KKKT Dayosisi ya Kaskazini usharika wa Sanya juu kwa ajili
ya kununulia gari la kutoa huduma za neno la Mungiu kwa kikundi cha Uamsho.
Akizungumza
wakati wa harambee hiyo Mbowe alisema kuwa ifike mahali wananchi wasitoe nafasi
kwa kazi za kibinadamu zikachafua kazi ya Mungu,ambapo alisema kuwa shida
imewafanya watu wengi kutenda matendo yasiyompendeza Mungu kwa ajili ya
kujitafutia kipato.
Alisema
kuwa vitendo vya ushirikina vimekidhiri nchini,huku viongozi wakubwa wan Nchi
wanaotegemewa kuongoza nchi wakitegemea kuongozwa na vitendo vya
kishirikina,hususani wabunge wa jamhuri ya Muuungano ambapo wanategemea
ushirikina kuweza kupata nafasi hizo za kuwawakilisha wananchi.
Mbowe
ambae pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)Taifa alisema kuwa zaidi ya asilimia 80 ya wabunge wa Nch wanategemea vitendo vya
kishirikina,na wengi wanatoka vyama mbali mbali vya siasa na ukikaa nao ndipo
utaweza kugundua kwa matendo yao hususani na katika kuongoza na kuchaguliwa
yanategemea nguvu za giza.
“Shida
imewafanya wananchi kujiingiza katika vitendo viovu ikiwemo kuanzisha makanisa
ili kujipatia vipato,viongozi wa dini tunawategemea sana,katika mambo mengi ya Nchi hii ikiwemo
kusaidia kupatika kwa viongozi wanaoweza kuiongoza hii Nchi”Alisema Mbowe.
Harambee hiyo ilihudhuriwa na vioongozi
mbalimbali wakiwemo wale wa dini wa
siasa,ambapo kwa upande wa Mbunge wa Jimbo hilo Agrey Mwandry hakuwezi kufika,licha
ya kualikwa na kutajwa jina lake wakati wa utambulisho wa wageni
walioalikwa,bila ya kuwepo kwa muakilishi wake.
Miongoni
mwa wanasiasa waliokuwemo kwenye harambee hiyo alikuwemo pia mgombea wa ubunge
wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chadema Humpfrey
Tuni ambae kura zake hazikutosha akichangia kiasi cha shil milioni moja kwa
ajili ya ununuzi wa gari hilo.
Jumla
ya zaidi ya shilingi mill 14 ziliwezeza
kupatikana kwa ajili ya ununuzi wa gari hilo.ambapo lengo lilikuwa ni kupata
kiasi cha shilingi million 50 katika kununua gari hilo la kutolea huduma za kiroho.
No comments:
Post a Comment