Monday, May 14, 2012

WANANCHI WILAYANI HAI WALIA NA WIZI WA PEMBEJEO ZA KILIMO
Mkuu wa Wilaya ya Hai Novatus Makunga.

Baadhi ya wananchi wa Kata ya Hai Mjini Wilayani Hai wamelalamikia upotezo wa vocha 135 zenye dhamani ya zaidi ya shilingi million 9 ambazo zilikuwa zigawanywa kwa wakulima wa kata hiyo.
Wakizungumza na Dira ya Leo mwenyekiti wa mtaa wa gezaulole kwenye kata hiyo Simon Mnyampanda amesema kuwa kwenye kikao cha WDC cha tarehe 06/03  walisomewa  agenda kuu ambayo ilikuwa ni vyocha za pembejeo ambazo mtendaji alisema kuwa kata hiyo imepata vocha 550.
Amesema kuwa hoja ya idadi hizo za vocha iliyosomwa na Mtendaji wa Kata hiyo Neema Lema iliungwa Mkoni pia na Diwani wa kata hiyo jafar kiure,ambapo baada ya kufuatilia idadi iliyotolewa na Serikali kwenye Kata hiyo kutoka Serikalini ni vocha zipatazo  685.
Hata hivyo dira ya leo imewasiliana na Mwenyekiti wa vocha kwenye kata hiyo Abuu Kimaro hakupenda kutoa ushirikiano kuhusiana pamoja na afisa mtendaji neema lema baada ya kupiga simu zao za mkononi bila kupatikana.
Kwa upande wake mkurugenzi wa halm ya hai Melkizedeki humbe alisema kuwa hana taarifa ya wizi huo wa vocha za pembejeo,huku akisema suala hilo atalifuatilia.
Naye diwani kata ya mjini jafari kiure alipoulizwa kuhusiana na upotevu huo wa vyocha alisema yeye hausiki kwenye kutoa  taarifa ya vocha kwa sababu siyo mtendaji,ila kama kuna udanganyifu ni suala la kuhoji,huku akisema hafahamu idadi ya vocha zilizogawanywa kwenye kata yake .
Hata hivyo dira ya leo ilifanikiwa kuinasa barua iliyokuwa im etoka halm ya hai ambayo ilikuwa inahusu mgao wa vocha za pembejeo kwa mwaka 2011/12 kuonesha kuwa idadi ya vocha ni kwenye kata hai ni 685.

No comments:

Post a Comment