Monday, April 23, 2012

CWT YALIA NA MADAI YA WAALIMU KILIMANJARO 
Katibu wa Chama cha waalimu Tanzania Mkoa wa Kilimanjaro Nadhanael Mwandete akizungunza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na amadai ya waalimu.

Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari,wa kwanza kushoto,Charles Lyimo Nipashe,aanayefuata Rehema matowo wa Mwananchi,Enos Masanja wa Star tv,Samwel Shayo wa Radio Sauti ya Injili ,aliyevaa t shirt ya njano ni Zephania Reanatus na Mpiga picha wa Itv aliyesimama Roberth Minja.

Kuanzia kushoto,Charles Lyimo nipashe,Enos Masanja Star tv,Reehema matowo Mwananchi,Samweli Shayo,zephania Renatus na Mpiga picha wa itv Robrth Minja wakimsikiliza Katibu wa CWT hayupo pichani.



Waalimu wa Mkoani Kilimnjaro wamelelamikia kutolipwa malimbikizo ya madai yao ya mishahara na yasiyo ya mishahara zaidi ya shilingi billion 2.6 huku Wilaya ya Same ikiongoza kwa Wilaya ambazo waalimu hawajalipwa kabisa madai yao.

Akizungumza na waandishi wa habari Katibu wa Chama cha waalimu Tanzania(CWT)Mkoa wa Kilimanajro Nadhanael Mwandete alisema kuwa madai hayo yalikwisha lipwa kwa mara ya kwanza lakini hayakuwa na tija huku baadhi ya Wilaya Kama Same zikisahaulika kulipwa.

Alisema kuwa maadai hayo kwa walimu Wilayani Same ni zaidi ya shilingi milioni 978 ambayo yanahusisha madai ya mishahara na yasiyo ya mishara,kwa walmu 107 huku Wilaya ya Moshi Vijijini ikidai zaidi ya million528.

Madai wanayodai walimu ni pamoja na makato ya mishahara,waalimu kupanda madaraja na kuendelea kulipwa mishahara ya zamani,likizo,matibabu pamoja na wanapoamishwa  sehemu zao za kazi,madai ambayo hadi February mwaka huu yangepaswa yawe yamelipwa.
               
Mwandete alisema kuwa Serikali ilikwisha hakikisha madai hayo ya walimu kwenye Wilaya zote za Mkoa wa Kilimanjaaro kwa kushirikiana na Makatibu wa CWT lakini cha kushangaza wapo walimu ambao madai  yao hadi sasa hayajalipwa.

“Serikali ililipa madai ya walimu yanayohusiana na mishahara tena kidogo lakini yale ambayo hayahusiani na mishahara yakiwa bado ambapo hata billion 2 haikufika,na mimi nikiwa kama Katibu wa chama cha waalimu nimekuwa nikipokea malalamiko kila kukicha wakilalamikia hali ngumu”Alisema Mwandete.

Alisema kuwa sababu ambayo Serikali imekuwa ikijitetea kutokana na kutolipa madai hayo ni baada ya kuruka ukurasa wa Wilaya ya Same,lakini pia wapo ambao wamekuwa wakikatwa mishahara tangu miezi ya oktoba hadi February wamekuwa wakipunjwa mishahara yao.

Alisema waalimu ambao wamekatwa mishahara kwa kupunjwa wanafika 19 ambao wanatoka wilaya ya Moshi Manispaa na Hai ambapo tangu mwezi oktoba hado February hawajalipwa mishahara yao yote,kama wanaolipwa laki 7 kujikuta wanalipwa laki 3.

Alisema kuwa tatizo la madai ya waalimu ya mishahara na yasiyo ya mishahara yapo kila Wilaya lakini Wilaya ya Same ndo limekuwa tatizo kubwa zaidi.

Alisema kuwa hali hiyo itawafanya waalimu waichukie serikali yao kutokana na kutoijali licha ya huduma ambayo imekuwa ikiyoa kwa Serikali.

Hata hivyo alisema  Mkoa wa Kilimanjaro umekuwa ukisifiwa sana kwenye suala la maendeleo ya elimu hivyo sababu kama za madai ya malimbikizo ya walimu n zinaweza kuchangia kushuka kwa kiwangp cha elimu kwa sababu madai waalimu wanayodai ni ya msingi.

No comments:

Post a Comment