Wednesday, March 6, 2013

MATOKEO YA UCHAGUZI WA KENYA 2013,CORD WAWALAMIKA

Kenyan Prime Minister Raila Odinga (L), Vice President Kalonzo Musyoka (C) and Trade Minister Moses Wetangula gesture at supporters in Nairobi on December 4, 2012 after agreeing to form a powerful alliance as running mates in presidential elections due in March 2013. The former rivals along with leaders of 10 other smaller parties, signed an agreement in front of thousands of supporters to form the Coalition for Reform and Democracy (CORD) party. Odinga is widely tipped to be the presidential candidate with Musyoka as his deputy, although no formal announcement was made. AFP PHOTO / TONY KARUMBA (Photo credit should read TONY KARUMBA/AFP/Getty Images)


Viongozi wa muungano CORD wamelalamikia namna matokeo ya kura yanavyotolewa, huku waangalizi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki na wa Soko la Pamoja la COMESA wakitoa ripoti zao za awali.
Huku matokeo ya uchaguzi yakizidi kutiririka kutoka katika kituo cha kuhesabia kura jijini Nairobi, viongozi wa muungano wa CORD wamelalamika kwamba utaratibu unaotumiwa kutangaza matokeo hayo unatia shaka.
Kulingana na taarifa iliyosomwa na Kalonzo Musyoka, mgombea mwenza wa Raila Odinga, viongozi kutoka vyama vinavyounda muungano huo wameowaomba wafuasi wao kuwa watulivu wakati matokeo yote yanavyosubiriwa.
Kalonzo alisema kuwa bado wana uhakika wa kushinda katika uchaguzi na akaongeza kuwa endapo watashindwa wako tayari kusalimu amri.
Kauli ya CORD yanakuja wakati ambapo kinara wa mrengo wa Jubilee, Uhuru Kenyatta, anaonekana kuongoza katika matokeo ya awali yaliyotolewa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).
Hata hivyo, Kenyatta na mpinzani wake wa karibu Odinga wanamenyana vilivyo huku kila mmoja wao akiwa ametimiza zaidi ya kura milioni mbili.
Katika mkutano na waandishi wa habari, mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Bw. Isaack Hassan amewaomba wanasiasa wawe watulivu wakati huu wa kuhesabiwa kwa kura na akakiri kuwa kulikuwa na hitilafu Fulani za kimitambo ambazo zilichangia kucheleweshwa kwa matokeo.
Hata hivyo, mgombea mwenza wa muungano wa Jubilee, William Ruto, alisiifu IEBC kwa kuendeleza shughuli za uchaguzi kwa utaratibu unaofaa. Ruto amewashukuru Wakenya kwa kujitokeza kwa wingi ili kupiga kura siku ya Jumatatu.

No comments:

Post a Comment