Wednesday, March 6, 2013

COMESA, EAC WATOA RIPOTI YA AWALI.


  Wafuasi wa muungano wa CORD.
Wakati huo huo, tume ya wangalizi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki na mataifa wanachama wa COMESA imetoa ripoti yao ya mwanzo kuhusiana na zoezi nzima la uchaguzi.

Kiongozi wa ujumbe huo, Abdulrahman Kinana kutoka Tanzania, amesema kuwa uchaguzi wa Kenya uliendeshwa kwa njia ya kidemokrasia na kuisifu tume ya uchaguzi kwa kutekeleza wajibu muhimu kulingana na katiba.

Hadi kufikia majira ya jioni, kura bado zilikuwa zikihesabiwa na matokeo kamili yanatarajiwa wakati wowote. 

Kwa mujibu wa katiba, tume inayo nafasi ya kutoa matokeo yote katika kipindi cha wiki nzima tokea siku ya kupiga kura.
Mwandishi: Reuben Kyama/DW Nairobi

No comments:

Post a Comment