Sunday, March 10, 2013

MBIO ZA NYIKA TAIFA ZIMEFANYIKA LEO MJINI MOSHI; ARUSHA WATESA


 DICKSON MARWA AKIMALIZA
 WANARIADHA WA KILOMETA 12 KATUIKA MBIO ZA NYIKA
WANARIADHA WA KILOMETA 12 WALIPOANZA KUTIMUA MBIO

WANARIADHA kutoka mikoa mbalimbali nchini  jana walishiriki katika mbio za Taifa za Nyika zilizofanyika Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro,huku washindi waliotawa mbio hizo wakitoka mikoa ya Arusha na Kilimanjaro.

Mashindano hayo ambayo yalifanyiika katika uwanja wa moshi wa Gofu yalishirikisha Washirikisha wapatao 100 kutoka mikoa ya Mwanza, Arusha, Manyara, Singida, Mara, Zanzibar, mbeya, Dar es salaam na Kilimanjaro,ambapo Kilimanjaro iliweza kutoa mshindi wa Kilomita 12.

Pia wanariadha wengine waliofanya vizuri kwenye mbio hizo wanatoka Mikoa ya Arusha ambao walitawala kwa kuchukua nafasi za juu katika mbio za kilomita 12, 8 na 6,ambapo jumla ya wakimbia 100 walishiriki.

Kwenye Mbio za Kilimita 6  za wanawake wenye umri chini ya miaka 20 washindi walikuwa ni Anjeline Irene 21:19;57, Selina Amosi 21:31:86, Fadhila Salum wote kutoka Arusha mbio za km 8 wanawake Jaeldine Sakilu (JWTZ-Arusha) 27:00:34, Zakia Mrisho  (Arusha) 27:24:58 na Catherine Lange (Manyara) 28:12:91.

Kwa upande wa wanaume kwa mbio za kilomita 8 washindi walikuwa ni  Dotto Ikangaa 23:53:95 JWTZ-Arusha, Joseph Theophil Mbulu 23:56:41 na Mohammed Ally 24:13:54 JWTZ- Arusha huku mbio za km 12 wanaume akichukua Dickson Marwa 36:34:52 kutoka Holili-Kilimanjaro.

Rais wa Shirikisho la Riadha Taifa, (RT), Anthony Mtaka alisema kuwa madhumuni ya mbio hizo, ni kuandaa kikosi kitakacho iwakilisha Taifa katika mbio za Nyika za dunia zitakazofanyika Machi 24, nchini Poland pamoja na kuibua vipaji vya riadha nchini.

Alisema kuwa ili kuweza kufanya vizuri katika mashindano ya dunia ni lazima kuwepo na maandalizi mazuri kwa kuweka wachezaji kambini,kwa kuwapa mazoezi na majiribio ndipo Watanzania wataweza kufanya vizuri katika mbio zinazofanyika kimataifa.

 Anthony alisema kuwa chanagamoto kubwa katika kuandaa mashindano ipo katika kuwapata wadhamini kwani zoezi la kuwandaa wachezaji wataoshiriki katika mashindano inahitaji garama kubwa.

“Kwa mfano suala la timu ya taifa ya Riadha kushindwa kufanya vizuri RT, hatupaswi kulalamikiwa kwani sisi kama RT hatuna timu, na majukumu yetu ni kusimamia timu na kuhakikisha kuwa timu inapata huduma zote kabla ya mashindano”Alisema.

Mgeni Rasmi kwenye riadha za Nyika alikuwa ni Mkuu wa Chuo cha Polisi Moshi, Matanga Mbushi,kwa muda mrefu nchi yetu ya Tanzania kuwa washiriki katika mashindano mbalimbali badala ya kwua washindi hivyo wanariadha wanahitaji kufanya mabadiliko.

“Mimi chuo changu kimeandaa wanamichezo wapo 12,tunataka wawe mfano na baadae ikiwezekana tutawachukua wengine ili kuweza kuleta mabadiliko kwenye mchezo wa riadha”Alisema Mbushi.

Mmoja wa mwanariadha aliyeshiriki mbio za jana, Dickson Marwa, aliyeshinda mbio za km 12 mwanaume, alisema kuwa endapo kukiwepo na maandalizi mazuri wanariadha wataweza kufanya vizuri katika mashindano ya riadha ambapo yeye alisema yupo tayari kuiwakilisha nchi katika mbio za Poland.

Hata hivyo katika mashindano hayo ambayo yalikuwa na mchuano mkali mshindi wa kwanza alipokea zawadi mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha taslimu.
 

No comments:

Post a Comment