Sunday, June 17, 2012

            USAFIRI WA BODABODA UNAVYOKATISHA  MAISHA YA WANANCHI..
Wananchi wakimtazama mwendesha pikipiki maarufu kama bodaboda baada ya kugongwa na gari eneo Endask Wilaya ya Hanang Mkoani Manyara gari la abiria,hata hivyo mmiliki wa blogi hii aliweza kushuhudia ajali hiyo kutokana na gari hilo alilokuwa amepanda kumgonga mwendesha bodaboda huyo.

Sehemu ambayo pikipiki hiyo iliingia kwa upande wa gari kwa mbele na kusababisha kushindwa kuendelea na safari kwa masaa kadhaa hivi.

Hapa askari wa usalama barabarani wakiwa kazini.

Ajali hii ilikuwa mbaya sana asikwambie mtu,watumiaji wa vyombo vya moto hususani pikipiki wanatakiwa kuwa makini sana pindi wanavyotumia vyombo hivyo,kwani ajali hii ilisababishwa na mwendesha pikipiki kuingia barabarani huku akiwa anazungumza na simu na kusababisha kugongwa.

No comments:

Post a Comment