Thursday, April 19, 2012

ZAO LA TUMBAKU KAHAMA LAENDELEA KUSHIKA KASI...

Mkulima wa Tumbaku akiwa shambani zao ambalo linadaiwa kupita mapato ya madini kwa sasa

PICHA YA ENEO LA MGODI WA BULYANHULU KAKOLA

 HALMASHAURI ya Wilaya ya Kahama imepitisha mpango wa bajeti ya sh bilioni 43.7 kwa mwaka 2012/2013 huku katika  mapato yake ya ndani yanayotarajiwa kuongezeka kwa asilimia 27.6 yakiongozwa na zao la tumbaku


Hali hiyo inadhihirisha wazi kuwa mapato hayo yanapiku yale ya migodi miwili ya dhahabu ya Bulyanhulu na Buzwagi inayomilikiwa na Kampuni ya African Barrick Gold Mine.
Katika bajeti ya mwaka huu, halmashauri hiyo, inatarajia kutumia kiasi hicho cha fedha ikiwa ni ongezeko la asilimia 1.5 kutoka  bajeti iliyopita kwa ajili ya matumizi ya kawaida, mishahara sambamba na miradi mbalimbali ya maendeleo.

Katika bajeti iliyopita hadi kufikia Machi mwaka huu, sh 13.6 sawa na asilimia 31.5 kati ya sh milioni 43.1 zilizopitishwa ndizo zimekusanywa.

Kwa mujibu wa Ofisa Mipango wa halmashauri hiyo, Duncan Thebas, fedha hizo ni pamoja na sh bilioni 4.9 kutoka vyanzo vya mapato ya ndani, ikiwemo migodi ya dhahabu ya Bulyanhulu na Buzwagi pamoja na makampuni ya kununua zao la tumbaku.

Aidha, katika taarifa hiyo, alisema kuwa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu itachangia jumla ya dola za Marekani laki nne sawa na wastani wa sh milioni 600 huku makampuni ya kununua zao la tumbaku yakilipia ushuru wa sh milioni 720.

Kutokana na mpango huo wa bajeti, zao la tumbaku  ndilo linaloongoza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika mapato ya ndani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kahama tofauti na jamii inavyodhani kuwa dhahabu ndiyo inayochangia mapato makubwa,

 
 

No comments:

Post a Comment