Thursday, April 12, 2012

BABA MZAZI WA ELIZABERTH MICHAEL KIMEMETA LULU,AFUNGUKA KUHUSU MWANAE KUHUSISHWA NA SHITAKA LA MAUJI YA MSANII MWENZAKE MAREHEMU STEVEN KANUMBA.
MICHAEL EDWARD KIMEMETA AMBAYE NI BABA MZAZI WAELIZABERTH MAARUFU KAMA LULU


Mwigazaji wa Kike Elizaberth Micahel Kimemeta(katikati) akitoka Mahakamani jana

Baba mzazi wa Muigizaji wa kike wa filami nchini Elizabeth Michael Kimemeta maarufu kama Lulu ambaye anahusishwa na kifo cha msanii na muandaji wa filamu nchini Steven Kanumba amelezea kushtushwa juu ya taarifa za kifo hicho pamoja na mwanaye kudaiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na muigizaji huyo nguli.

Baba wa Elizabeth Michael ambaye alijitambulisha kwa jina la Michael Edward Kimemeta(49)mzaliwa wa Wilayni Rombo Mkoani Kilimanjaro alisema kuwa alimtambua Steven Kanumba kama mwalimu wa mtoto wake lulu,lakini hakuamini baada ya kupata  taarifa za kifo cha kanumba huku mwanae akidaiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Kanumba.

Msanii  huyo wa kike Elizaberth Michael alifikishwa mahakamani april 11 akikabiliwa na mashtaka ya mauaji ya msanii wa filamu Marehemu Steven Kanumba,ikiwa ni siku nne, tangu alipokamatwa mara baada ya kifo cha msanii huyo.

Alisema kuwa Elizaberth Michael alizaliwa tarehe april 17/1995 hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam ambaye alimaliza elimu ya  kidato cha nne katika shule ya sekondari ya  Midway  mwaka jana na hivi sasa anamamiaka 17.

“Umri wa Elizaberth bado alikuwa ni mwanafunzi ukilinganisha na umri wa marehemu Kanumba na hadhi yake katika jamii iliyodhibitishwa na mazishi yake kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu”Alisema

 Michael alisema kuwa ni vema polisi kuweka uwazi katika taarifa zao za uchunguzi kwa kuzingatia kuwa tukio hilo ambalo lilisababisha kifo cha Muigizaji Kanumba limejenga chuki na uhasama dhidi ya msaani wa kike Lulu na ndugu,marafiki na wapenzi wa Muigizaji ambaye sasa ni marehemu Steven Kanumba.

Alisema kuwa kilichomshtusha zaidi ni baada ya taarifa za polisi kusema kuwa ulitokea ugomvi kati ya Marehemu Steve Kanumba na Lulu,huku ikitajwa kuwa walikuwa wapenzi,huku akisema kuwa Lulu alikuwa bado ni mwanafunzi baada ya kumaliza kidato cha nne mwaka jana.

“Hatukutegemea kuwa kama Marehemu Kanumba angeweza kuwa na mahusiano na binti yetu kwanza ndiye tuliyekuwa tukimtegemea kwa kaisi kikubwa katika kuendeleza na kukikuza kipaji alichokuwa nacho mwanatu  Elizaberth”Alisema Michael.

Alisema Upelelezi unaofanyika kuhusu kifo cha kanumba umeegemea upande mmoja kutokana na Lulu na yeye kuwa na majeraha ya kuumizwa na Marehemu Kanumba,na marehemu  Kanumba kudaiwa ndiye aliyeanza kumshambulia Elizaberth.

“Ninaomba Wanasheria na wanaharakati wa haki za kibinadamu kuingilia suala hili kati na  kusaidia katika shtaka la mauaji linalomkabili mwanangu Elizaberth kwani tofauti na linavyochukuliwa kishabiki’Alisema

Hata hivyo alisema kuwa jamii inatakiwa kutambua mazingira ya tukio hilo,ambapo chanzo ilitokana na ugomvi uliopelekea tafrani na Lulu kumsukuma Marehemu Kanumba hali ambayo inaelezwa kuwa ilitokana na wivu wa kimapepenzi na hakukusidua kumuua hivyo yeye anashangaa mwane kuhusihwa na mashtaka ya mauaji.

Alielezea chuki ambazo zilizopo kwa jamii juu ya kifo hicho pia inatokana na jinsi viogozi mbalimbali wa nchi walivyotafsiri tukio hilo,hali ambayo pia inachoche uhasama na badala yake wangetakiwa kuiachia mahakama kufanya kazi yake na siyo kuhukumu kwa kusikiliza upande mmoja.

“Ushiriki wa mwanangu kuhusu mambo ya sanaa nilikwishapata wasiwasi na mama yake mzazi akawasiliana na Marehemu Kanumba ambaye alikuwa anamhakikisha usalama wa mwanae Lulu na kusema kuwa ataendele kubaki kama mwalimu..lakini leo nasikia ni mpenzi nilishtushwa”Alisema Kimemeta.

Katika hatua nyingine alitoa wito kwa wanasia,viongozi wa dini na wanaharakati,wasomi,kuanzisha mjadala mpana utakaohusiana na uhusiano wa Lulu na marehemu Kanumba pamoja na tukio lilisababisha kifo chake.

Hata  hivyo katika hatua nyingine Michael ameelezea kusikitishwa kwake baada ya  kushindwa kuuzuria mazishi ya kumuaga marehemu kanumba kutokana na chuki na uhasama kutoruhusu,ambayo mpaka hivi sasa mazingira hayaruhusu,lakini pindi yatakaporuhusu hata sita kufika nyumbani kwa marehemu Kanumba na kutoa pole.

 Suala hilo la mauaji ambalo anahusishwa lulu alisema kuwa familia haina la kufanya ila inamuachia Mungu kwa kuwa hukumu yake ni ya haki.

Michael alisema kuwa anaungana na watanzania wote kutoa pole kwa familia ya kanumba kutoa pole kwa msiba mkubwa ambao haukutarajiwa,na kusema kuwa kanumba alikuwa bado ni kijana mdogo aliyeonyesha umahiri kwenye sanaa na mpaka sasa amecha pengo kwa familia na Tanzania kwa ujumla.


No comments:

Post a Comment