Sunday, March 25, 2012


CCM yadai kukamata barua ya CHADEMA
  Kinamama wakimshangilia Mgombea Ubunge wa CCM Sioi Sumari katika  kijiji cha Ngongongare,Kata ya Maji ya Chai.

MPANGO wa siri wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa kuandaa makundi ya vijana watakaofanya fujo kupinga matokeo endapo mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Sioi Sumari atatangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi huo mdogo, umejulikana.

Mpango huo ambao upo katika barua inayodaiwa kuandikwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk. Willbroad Slaa, mbali na kuainisha makundi hayo pia imeelezea hofu ya Chama hicho juu ya kushindwa kwenye uchaguzi huo mdogo wa ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki. 

Barua hiyo iliyosomwa jana kwenye mkutano wa kampeni za mgombea ubunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Sioi Sumari na Mratibu wa Kampeni Mwigullu Nchemba ambapo alidai kwamba, Dk. Slaa amekuwa akiwashutumu viongozi wenzake kwa kutumia lugha za matusi kwenye uchaguzi huo mdogo. 

Alidai katika barua hiyo Dk. Slaa amewalalamikia kwa kutumia lugha chafu yakiwemo maneno ya kumkashifu Rais mstaafu Benjamin Mkapa hatua ambayo ilionyesha kutokukomaa katika siasa ikiwa ni pamoja na kukiweka chama hicho kwenye mazingira ya kushindwa.

 “Barua hii ninayoisoma mbele yenu inawaagiza Vincent Nyerere ambaye ni Meneja kampeni za CHADEMA, na Mbunge wa Karatu Mchungaji Israel Natse kujipanga kwa kuandaa makundi ya vijana wa kufanya fujo kupinga matokeo endapo mgombea wa CCM, Sioi Sumari atashinda.

“Sasa ili mchujue hawa watu ni hatari tayari wameingiza vijana wa kufanya fujo siku ya kutangaza matokeo kama walivyofanya Igunga ambako walishindwa kihalali kabisa,” alisema Nchemba wakati akisoma barua hiyo na kuongeza: 
Habari na Mwandishi wetu Arumeru.

No comments:

Post a Comment