Tuesday, March 27, 2012

                                                    ARUMERU KWAWAKA MOTO..

WAKATI kampeni za uchaguzi mdogo  katika jimbo la Arumeru Mashariki zikipamba moto katika duru ya lala salama,  jana umesambazwa waraka maalum ambao unakihusisha Chama Cha Mapinduzi (CCM), pamoja wanachama wake ambao ni wapambanaji wa ufisadi nchini.

Waraka huo ambao umesambazwa katika mitaa mbalimbali ya Wilaya ya Arumeru umewahusishaWaziri wa Afrika Mashariki Samuel Sitta, Naibu Waziri wa Ujenzi Dk. HarrisonMwakyembe, munge wa Kahama James Lembeli pamoja na Mbunge wa Same Anne Kilango,wakiwataka wananchi kuwa mamini na uchaguzi huo.

Warakahuo unasema kuwa wao kama makada mahiri ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), walikuwepondani ya chama chao tangu enzi za Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere,ambapo kwa wakati huo chama hicho kilikuwa kimbilio la masikini na wanyonge.

Warakahuo mbali na kuzagaa katika mitaa ya mji ya Arumeru na vitogiji vyake piaulikuwa ukigawiwa na katika mikutano ta CHADEMA iliyofanyika katika Kata yaNshupu, na hauna nembo yoyote ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) zaidi ya kupewaanuani ya kamati maalum.

Warakahuo ambao umewekwa picha ya viongozi hao walipokuwa katika ibada katika moja yaKanisa la  lililopo Kawe Jijini Dar esSalaam.

Akihutubiamikutano ya kumnadi mgombea Ubunge kupitia CHADEMA, Mwenyekiti wa Taifa wachama hicho Freeman Mbowe, amewataka wananchi wa jimbo hilo kulinda amani nautulivu siku ya uchaguzi kwa kumchagua Joshua Nassari.

Akihutubia mikutano ya kampeni iliyofanyika katika kata  za Nkoasenga, Nshupu, Nguruma, Ndoombo,Urisho na Shambarai Burka, Mbowe, alisema kuwa uchaguzi huo mdogo kumekuwa na vitendo vya hujuma kutoka kwa CCM ambapo hivi sasa wamekuwa wakiandaa makundiya vijana na kuwapiga wanachama wao.

Habari na Mwandishi wetu Arumeru





No comments:

Post a Comment