Tuesday, March 27, 2012

                           Nassari, akiomba kura

 


Mgombeaubunge kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joshua Nassari,amewataka wananchi wa Arumeru Mashariki kutoichagua CCM kama ishara yakutoridhiwa na mwenendo wa chama kwa kushindwa kutoa huduma za maendeleoikiwemo maji na umeme.

Alisemakukosekana kwa huduma za jamii kama vile ukosefu wa umeme, elimu bora, afya,maji na migogoro ya ardhi,  sasa ni fursaya pekee kwa wananchi wa jimbo hilo kukataa ahadi mpya za chama tawala CCM na badalayake wahoji utekelezaji wa ahadi za chaguzi zilizotangulia.

 Aidhamgombea huyo ameulinganisha uchaguzi huo kuwa ni sawa na mapambano baina yagiza na nuru, haki dhidi ya dhuluma, haki dhidi ya rushwa na umaskini dhidi yautajiri, huku akidai kuwa CCM kimekuwa kikitumia fedha, kuvunja hakikuwadhulumu wapiga kura haki yao ya msingi kumchagua mgombea wanayemtaka.


                             Mwandishi wetu Arumeru

No comments:

Post a Comment