Wednesday, March 6, 2013

BAJAJI ZA WAJAWAZITO ZASHINDWA KUPUNGUZA KERO KWA WAKINA MAMA WAJAWAZITO


Kulia ni mganga mkuu wa kituo cha afya cha Ikizu Dk. Abahehe Kanora katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara, akionesha bajaji ya Kikwete ikiwa imetolewa kitanda cha kubeba mjamzito, kutokana na kushindwa kukitumia kwa ubovu wa barabara na haikati kona upande wa kushoto.

Wilaya ya Bunda ina kata 28 kati ya hizo kata 4 tu ndio zina vituo vya afya kama Ikizu, Manyamanya na Kasuguti vituo hivyo vina Bajaji ya Kikwete lakini hazitumiki kwa ubovu wa barabara, baada ya kutoa kitanda hicho wanatumia pikipiki kwenda kuchukua dawa wilayani.habari na Kalulunga Blog

No comments:

Post a Comment