Monday, October 22, 2012


MAHAFALI YA KIDATO CHA NNE SEKONDARI YA MAMA CLEMENTINA WAZAZI NA WAPEWA SOMO.


Mwenyekiti wa shirika la mama clementina Foundation akitoa nasaha zake kwenye mahafali hayo.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi,Betty Mkwasa akimkabidhi mmoja wa wahitimu zawadi.

                                                                     
                                                 Rodrick Mushi,Moshi.
Kutokana na tatizo la uhaba wa wataalamu wa  fani zinazohitaji masomo ya sayansi nchi jitihada mbali mbali imeelezwa kuwa zinahitaji kuanzia kwa wazazi kushirikiana na waalimu katika kuwashauri wanafunzi kuchagua  michepuo ya kusoma ili kusaidia kuondokana na tatizo hilo.
Akizungumza kwenye mahafali ya kidato cha nne ya shule ya sekondari Mama Clementina Foundation mwenyekiti wa shirika la Mama Clementine Foundatin  Maria Josephine alisema nchi ina tatizo la wataama kama Madaktari,mafamasia,wataalamu wa kilimo,wahasibu,maafisa biashara pamoja na fani nyingin zinazohitaji elimu ya sayansi.
Alisema kuwa wanafunzi wengi wamekuwa wakisoma masomo ambayo inakwua rahisi kwao kuweza kufaulu huku akitolea mfano michepuo kama ya Mahusiano ya Umma,Maendeleo ya Jamii utawala na michepuo mingine huku uhaba ambao umekuwa wa wataalamu ukiendelea kuongezeka.
Maria Alisema kuwa kutokana na tatizo hilo kuwa kubwa mikakati mbalimbali inahitajika ikiwa ni pamoja na kuinua na kuyapa kipaumbelea masomo ya sayansi na biashara,na wazazi kuwa karibu kuwaeleza faida za kuchukua michepuo hiyo ambayo pia imekuwa na nafasi kubwa ya ajira.
“Tatizo linalokabili nchi yetu ni tatizo la uhaba wa wataalamu,na wataalamu wanaohitaji ni muhimu na ili nchi iendelee lazima Nyanja hizo wawepo wataalamu wa kutosha hivyo suala hilo Serikali na wadau wengine kama wazazi na waalimu wanapaswa kushiriana kulimaliza”Alisema
Katika hatua nyingine alisema tatizo hilo linanzia mashuleni kwa wanafunzi kushindwa kufanya vizuri katika masomo ya sanyansi kama phisikia,kemia baologia na hesabu huku idadi ya wanaoshidnwa kufanya vizuri wakiwa ni wasichana,ambapo wanafuzni ambao wamekuwa wakifanya vizuri ni wale wanaosoma shule binafsi.
Kwa upande wake Mgeni rasmi kwenye mahafali hayo Mkuu wa Wilaya ya Bahi Betty Mkwasa alitoa wito kwa wamiliki wa shule binafsi kuwa na tabia ya kujitolea kuwasomesha baadhi ya watoto ambao wazazi hawana uwezo au yatima kama ambavyo shule hiyo ya mama Clementina imekuwa ikifanya.
“Kuna wamiliki wa shule binafsi ambao wamewasahau kabisa watoto maskini lakini ukweli ni kwamba ukimsaidia maskini utapa Baraka kwa Mungu lakini pia umesaidia kujenga taifa kwani motto mmoja unayemsaidia anaweza kuja kuikomboa jamii yake”Alisema Mkwasa.
                                                                         Mwisho

No comments:

Post a Comment