Monday, July 9, 2012

UMOJA WA MATAIFA WATOA BILL 11KUWEZESHA KIWANDA CHA MADAWA ARUSHA. 


Umoja wa nchi za Ulaya umetoa kiasi cha Sh bilioni 11 kwa ajili ya kukiwezesha  kiwanda ch kutengeneza madawa ya binadamu cha TPI kilichopo njiro Mkoani Arusha, ambapo kitaanza kutengeneza dawa za kurefusha maisha kwa waathirika kwa ugonjwa wa ukimwi .

Hayo yalisemwa  na Balozi wa Nchi za Umoja wa Ulaya, Timoth Clarke wakati alipokuwa akielezea nchi za umoja wa ulaya zinavyojitahidi kutoa misaada mbalimbali ya kimaendeleo hususan katika sekta ya afya, elimu ,vifo vya kinamama na watoto .

Alisema katika kiwanda hicho kumeanzishwa kitengo cha kutengeneza dawa za kurefusha maisha kwa waathirika wa   VVU na kwamba kiwanda hicho kama hakitafunguliwa ,Taifa linaweza kupoteza nguvu kazi ambazo zinatokana na wale wagonjwa waliokumbwa na maambukizi hayo na kuongeza kuwa kupatikana kwa dawa hizo nchini kutawezesha wale walioathirika na ugonjwa huo kuendelea na shughuli mbalimbali za kijamii ambazo zinaweza kuinua uchumi wan chi.

Alisema si busara kwa nchi kuwatenga waathirika wa ukimwi sehemu mbalimbali bali jamii inatakiwa kuwapa TANZANIA ni nchi mojawapo inayojitahidi kutokomeza maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kwa kutumia kampeni mbalimbali ikiwemo kupunguza vifo vya kinamama na watoto vinavyotokana na ugonjwa huo.

No comments:

Post a Comment