Friday, July 27, 2012


 MFANYABIASHARA AUAWA KWA WIVU WA MAPENZI.

Kamanda wa mkoa wa kipolisi Tarime na Rorya  Justus Kamugisha
 
MFANYABIASHARA mmoja katika kitongoji cha Nyangoto kataya Matongo
wilayani Tarime Mgaya NyamhangaSindo(28)ameuawa kwa kuchomwa visu
sehemu tano maeneo  mbalimbali ya mwili kutokana na wivu wa mapenzi.
Tukio hilo limetokea julai 24,majira ya kati ya saa 1.45 na saa 2:00
mwaka huu  usiku nyumbani kwa Marwa Machugu katika mtaa huo alipokuwa
ameenda kununua mawe yanayodaiwa ya dhahabu limethibitishwa na
polisi,na kiongozi wa mtaa huo.
Mwenyekiti wa kitongoji hicho Chacha Kichere alimtaja mtuhumiwa wa
tukio hilo kuwa ni Ngewa Masicho Magau (39)ambaye anashikiliwa na
polisi  chanzo kikiwa ni ujumbe wa simu unaodaiwa kutumwa na Sindo
kwenye simu ya mkewe Otaigo Ngewa Masicho .
Alimchoma visu sehemu tano ikiwemo tumboni mara mbili,kifuani,jichoni
na mgongoni na kuanguka chini akiwa amepoteza fahamu.
“Ujumbe uliokutwa kwenye simu ya mke wa mtuhumiwa unaodai mbona
hatukukutana  unipe ule mzigo”alifafanua na kuongeza kuwa”kulikuwa na
hisia za kuwa anauhusiano wa kimapenzi na mke wa mtuhumiwa na hata
ndoa yao ilikuwa na mgogoro”alisema Mwenyekiti.
Kabla ya tukio hilo alidai Sindo alipigiwa simu na rafiki yake Marwa
Machugu wakanunue mawe ya dhahabu “wakiwa nyumbani kwa Machugu ghafla
mtuhumiwa alitokea na kuanza kumshambulia kwa kisu huku rafiki yake
akiwa hatoi msaada’alisema.
Hata hivyo alidai Machugu ambaye alimpigia simu anahusishwa na mpango
huo na kuwa ndiye alimpigia simu na kumkuta mtuhumiwa eneo hilo,na
hata hayo madini hayakuwepo.
Alibainisha kuwa majilani ndio walitoa msaada wa kutaka kumwokoa ,hata
hivyo alifia njiani wakati wanampeleka kituo cha afya cha Goldwill
Foundation kituo cha Nyangoto na kulazimika kupeleka mwili wa marehemu
kituo cha afyua cha Sungusungu ambacho ni cha serikali.
Hata hivyo alisema mtuhumiwa baada ya kuona wananchi wamejitokeza kwa
wingi alikimbilia kituo cha polisi akiwa na kisu chake  na
kujisalimisha na  anashikiliwa kuhusiana na tuhuma hizo.
Mmoja wa majilani wa mtuhumiwa jina tunalo aliliambia gazeti hili kuwa
mtuhumiwa siku ya tukio kwa nyakati tofauti alisikika akidai ataua mtu
bila kumtaja mtu mwenyewe.
Kamanda wa mkoa wa kipolisi Tarime na Rorya  Justus Kamugisha alisema
mtuhumiwa natarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote,huku mke wa
mtuhumiwa akisaidia polisi kutokana na kuhusishwa na tukio hilo.
Wakati huo huo alisema Waitara Sebuti Masiane(42)mkazi wa kijiji cha
Nyantira kata ya Nyansincha amekufa baada ya kunywa pombe aina ya
gongo ambayo inadaiwa ilikuwa na sumu na mtuhumiwa Mirama Nyangira
anashikiliwa kwenye kituo kidogo cha Nyamongo.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment