LULU APANDISHWA KIZIMABANI KWA MARA YA PILI MAHAKAMA YA KISUTU
Hali ilikuwa hivi Ezeckiel Michael aliambatana na askari mbalimbali wa Magereza ambao walikuwa wanamlinda asipata ghazabu kutoka kwa watu mbalimbali waliokuwa mahakamni hapo. |
Hapa akiwa ameambata na askari wa Kike. |
Gari la Magereza lililomleta Lulu na kumrudisha Magereza hadi hapo Mei 7 kesi hiyo itakaposikilizwa tena. |
Askari waliokuwa wameizunguka mahakama ya Kisutu wakiwa wamevalia mikanda iliyojaa mabomu |
Kamishna wa tume za haki za binadamu Joacquine De-Mello leo
amejitokeza katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu akiambatana na Mawakili
wengine wa kujitegemea kumtetea msanii wa sinema Elizaberth Michael maarufu kama Lulu.
Akilitaja jopo la Mawakili wanaomtetea lulu wakili wa
kujitegemea Kenedy Fungamtama alisema kuwa mama De Mello ni miongoni ,mwa
mawakili pamoja na Furgence Massawe na Peter Kibatala hata hivyo hawakuongea
mahakamani hapo.
Wakili wa Serikali Elizaberth Kaganda alidai kuwa kesi
imekuha kutajwa hata hivyo upelelezi haujakamilika na kuomba tarehe nyingine
kutajwa na kupangwa kutajwa Mei 7.
Hali ilikuwa tofauti ba
ilicvyotarajiwa Lulu leo alikuwa katika huzuni wa hali ya juu huku askari
magereza wakiwa wamevalia mikanda yenye mabomu ya machozi ikiwa ni katika
kukabilia na rapsha ya aina yeyote ambayo ingeweza kutokea .
Kitu kingine ni kwamba msanii
huyo alifika akiwa amevalia gauni refu na mtandio wake mwekundu walitu walijaa
lakini siyo kwa wingi ambao wengi walitarajia kutokana na umaarufu alio
nao Lulu hata kabla ya kufikwa na tuhuma hizo za kesi ya mauaji ya
aliyekuwa Msanii nyota wa Filamu nchini Steven Charles Kanumba.
No comments:
Post a Comment