Friday, March 16, 2012

CHUO  CHA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI ARUSHA(AJTC) CHAFANYA MAHAFALI YAKE YA NNE.
Viongozi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji(AJTC)wakiwa pamoja na Mgeni Rasmi wa tatu kutoka kushoto,
ambaye ni mwanahabari Mkongwe nchini na mkufunzi kutoka shirika la utangazaji la Uingereza Joseph Msami,wa pili kutoka kushoto ni Mkurigenzi wa mafunzo wa  Chuo hicho Joseph Mayagilla.

\Wahitimu wakiimba wimbo kwa huzuni mbele ya wagenu na wanafunzi wanaobaki chuoni(hawapo pichani)

Mkurugenzi wa Mafunzo Joseph Mayagille akiwatoa neno kwa wahitimu.

Mgeni Rasmi Joseph Msami  akitoa Nasaha zake kwa Wahitimu

WAKAGUZI CREW WAKIWA KAZINI

BURUDANI MBALIMBALI ZILIKUWEPO,HAWA NI WANACHUO WENYE VIPAJI VYA PEKEE AMBAO WANATAMBULIKA KAMA INTERNET ARMY.



CHUO  CHA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI ARUSHA(AJTC) CHAFANYA MAHAFALI YAKE YA NNE.


Chuo cha uandishi wa habari na utangazaji cha Arusha (AJTC) kimefanya mahafali yake ya nne kwa wahitimu wa ngazi ya cheti na Diploma ambapo wahitimu wapatao 70 wa ngazi ya cheti walitunukiwa vyeti pamoja na 7 wa ngazi ya diploma.

Mahafali hayo yalifanyika kwenye ukumbi wa PPS uliopo jijini Arusha,ambapo mgeni rasmi kwenye mahafali hayo alikuwa  ni mwanahabari Mkongwe nchini na mkufunzi kutoka shirika la utangazaji la Uingereza Joseph Msami.

Kwenye mahafali hayo wanafunzi waliomaliza mafunzo ya ngazi ya Cheti Samweli Dida na Jackline Joel ambao walifanya vizuri walipata nafasi ya kuendelea na masomo yao ya diploma bure,kwa mujibu wa vigezo vilivyowekwa na chuo.

Lakini pia sio tu kwa wanafunzi wa ngazi ya cheti waliopata nafasi ya masomo bure pia waliomaliza diploma na kufanya vizuri,akiwemo Onesmo Mbise,Jackline Heriel na Prisca Mnzava walipata nafasi ya kufanya kazi kwenye chuo hicho,ambao watapewa mafunzo ya miezi mitatu kabla ya kuanza kazi.

Mkurugenzi wa mafunzo wa chuo cha Arusha Joseph Mayagille alisema wapo wanafunzi wenye uwezo ila waliochaguliwa wana uwezo mkubwa na kuona ni bora kuwabakisha chuoni hapo kwa kusaidia kuwapika wanahabari wapya na wao kujipatia ajira.

Kutokana na tatizo la ajira alisema kuwa chuo hicho kimekwisha anzisha utaratibu wa kutoa mafunzo ya ujasiriamali,ili kuwawezesha wahitimu kuibua miradi na kuwa na vipato.

Kwa upande wake Mgeni rasmi kwenye mahafali hayo,Msami alisema kuwa wahitimu hao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kuweza kufanikiwa malengo yao waliojiwekea na kuepuka kujiingiza kwenye matendo maovu yanayoweza kuwa chanzo cha kushindwa kufikia malengo.

Alisema kuna tatizo kubwa la wanafunzi wa vyuo kutajwa na taasisi mbalimbali kuwa vimekuwa vikiongozwa kwa wanafunzi kuwa na maambuzi ya Ugonjwa wa UKIMWI,jambo ambalo ni hatari kwa taifa na maendeleo ya mwanachuo mwenyewe.

Habari na picha zimewekwa na Rodrick Mushi wa Blog ya Tanzania leo.




No comments:

Post a Comment