Tuesday, October 9, 2012

 MWENYEKITI WA CCM ANGOLEWA MADARAKANI NA WANANCHI.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Hai akizungumza kwenye mkutano na wananchi wa kijiji cha kwasadala.

Mwenyekiti aliyengolewa madarakani Erenest Samwel akijitetea baada ya kusoma kwa tuhuma zilizokuwa zinamkabili.

Wananchi wakifuatilia kwa makini mkutano wa kumuondoa madarakani mwenyekiwa wa kijiji
rodrick mushi.

Mgogoro uliokuwa umedumu kwa muda mrefu baina ya Mwenyekiti wa kijiji cha Kwa sadala Erenest Samwel (CCM) na wananchi,jana ulifikia kikomo baada ya kufanyika kwa mkutano mkuu na wananchi kumkataa mwenyekiti kuendelea kubaki madarakani kwa kupiga kura za kutokuwa na imani naye.

Mkutano huo ulilazimishwa kufanyika na wananchi baada ya uongozi uliokuwa umetoka Wilayani kutaka kuhairisha mkutano huo wa kupiga kura za kutokuwa na imani na Mwenyekiti kwa madai ya akidi haijatimia kitu ambacho wananchi walikipingana nacho.

Baada ya mzozo wa hapa na pale hatimaye wananchi na uongizi Uongozi wa Wilaya kupitia kwa katibu tawala Mpotwa walikubalina kupigwa kwa kura za kutokuwa na imani naye ambapo malalamiko ya Mwenyekiti yalisomwa na kutakiwa kuyatolea ufafanuzi kabla ya kufanyika kwa zoezo la kura za abaki madarakani au aondoke.

Mmoja wa wananchi akizungumza kwenye mkutano huo Haji Mwasha alimtaka Katibu tawala aliyefika kwenye kijiji hicho,kutoa fursa ya mawazo na mamuuzi ya wananchi kusikilizwa na kufanyiwa kazi ili kuondoa dhana ambayo mwenyekiti amekuwa akiwatisha wananchi kuwa ameshawahonga viongozi wa Wilaya.

Wananchi wakionekana kuwa na jazba kwa madai ya matendo ya mwenyekiti,kura 154 ziliweza kumkataa kutoendelea na uongozi,huku kura 125 zikikubali aendelee kubaki madarakani  hivyo kwa matokeo hayo kumfanya mwenyekiti kukosa sifa ya kuendelea kuongoza.

Diwani wa Kata ya Masama Kusini Issa Kisanga,alisema kuwa miongoni mwa tuhuma zilizomuondoa mwenyekiti huyo madarakani ni pamoja na kuuza maeneo ya wazi kiholela,kuingiza kijiji kwenye mgogoro na kanisa,kutoa lugha chafu kwenye Mikutano ya hadhara,pamoja na kutofanya mikutano ya kusoma mapato na matumizi.

Alisema baada ya hatua hiyo kufikiwa kilichobaki ni wananchi kusubiri uongozi wa Wilaya  kutangaza taratibu za kumpata mwenyekiti wa kijiji wa muda kwa ajili ya kuongoza kijiji huku kukisubiriwa kutangazwa kwa uchaguzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji hicho aliyevuliwa uongozi Erenest Samwel alipopewa nafasi ya kujibu tuhuma mbalimbali alizokuwa anatuhumiwa nazo na wananchi,alipinga baadhi ya malalamiko kama ya uuzaji wa maeneo,huku akisema kuwa malalamiko mengine ni ya kupandikizwa.

                                                    Mwisho

No comments:

Post a Comment