WAANDISHI wa habari washauriwa kuandika Makala.
Waandishi wa habari mkoani Kilimanjaro wanaohudhuria mafunzo hayo.
WAANDISHI wa habari washauriwa kuandika habari za Makala
makala na kutokuogopa
gharama na muda kwani makala
ni jamvi la habari linaloelezea jambo kwa
kina na linaigusa jamii moja
kwa moja.
Ushauri huo umetolewa na
mhadhiri wa chuo kikuu cha mtakatifu
Augustino Peter Mutaba wakati
akitoa semina kwa waandishi wa habari
mkoani Kilimanjaro juu ya
uandishi wa makala iliyoandaliwa na muungano
wa vilabu vya uandishi wa
habari nchini(UTPC)na kuratibiwa na klabu ya
uandishi wa habari mkoani
Kilimanjaro(MECKI)
Mutaba alisema baadhi ya
waandishi huogopa kuandika makala kutokana na
gharama,muda na kutozingatia
utafiti juu ya jambo wanalotaka
kuliandika na kuwatoa hofu
kuwa ili makala iweze kuwa nzuri na yenye
kuigusa jamii moja kwa moja
inahitaji muda na kuigharamikia.
Aliongeza kuwa,makala kama
jamvi ni vyema ikazingatia mambo muhimu
yaliyokusudiwa kuandikwa na
ikawalenga jamii moja kwa moja badala ya
kuandika makala inayochochea
jambo Fulani ikiwemo vurugu.
Kwa upande wao washiriki wa
warsha hiyo ya siku nne waliushukuru umoja
wa vilabu vya waandishi wa
habari UTPC kwa kuwaandalia mafunzo hayo
pamoja na klabu ya waandishi
wa habari mkoani Kilimanjaro kwa kuomba
na kuratibu mafunzo hayo
kutokana na kutoa mwanga kwa washiriki
kufahamu namna ya kuandika makala isiyo ya
kichochezi.
No comments:
Post a Comment