Saturday, April 7, 2012

WIZARA  YA MALI ASILI NA UTALII KUSAIDIA SHINDANO LA MISS UTALII

             Waziri wa Mali Asili na Utalii Ezeckiel Maige.

 

WIZARA INAYATHAMINI MASHINDANO YA MISS UTALII
Wizara ya Maliasili na Utalii inaunga mkono Mashindano ya Miss Utalii na kuwa iko tayari kushirikiana na taasisi yoyote ya Sekta Binafsi ambayo itakuja na mikakati mizuri ambayo italenga katika kufanikisha maandalizi ya dhati ya kufanikisha mashindano hayo.
Msimamo huu umetolewa na Wizara kufuatia makala iliyochapishwa na gazeti la Mtanzania toleo la tarehe 7/4/2012 katika safu ya Wazo Binafsi yenye kichwa cha habari: ‘Serikali isichezee Shindano la Miss Utalii Tanzania’.
Wizara inasisitiza kuwa inathamini mashindano ya Miss Utalii na kamwe haitayachezea. Tangu shindano hilo lianze Wizara imekuwa ikiliunga mkono kupitia Bodi ya Utalii Tanzania (TTB). Pia Waziri wa Maliasili na Utalii amekuwa Mgeni Rasmi mara kwa mara katika hafla mbalimbali za mashindano hayo.
Wizara imekuwa ikihimiza Sekta Binafsi kutekeleza Sera ya Taifa ya Utalii kwa kubuni na kufanya shughuli mbalimbali zenye manufaa kwao na kwa taifa kwa ujumla, kama vile kuwekeza kwenye biashara ya hoteli , usafirishaji watalii na kutangaza utalii kwa njia mbalimbali.
Mashindano ya Miss Utalii ni njia moja wapo nzuri ya kutangaza utalii ndiyo maana Wizara inayaunga mkono. Ndiyo maana Wizara inaitaka Sekta Binafsi kuandaa mkakati mpya utakaolenga katika kufanikisha mashindano hayo na Wizara itatoa ushirikiano unaofaa.

George Matiko
MSEMAJI
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

No comments:

Post a Comment