Friday, April 6, 2012

WANANCHI WAKISIFU KIKUNDI CHA NDEKIRA KWA KUWA MKOMBOZI KWA   WANAMKE NA WATOTO.....    

Mwenyekiti wa Ndekira (kushoto)Catherina Bendict akiewa na wanachama wa kikundi hicho.

Wanachama wa Ndekira


 

KIKUNDI cha akina mama cha Ndekira kilichopo Kibosho Wilaya ya Moshi Vijijini Mkoani Kilimanjaro kimekuwa mkombozi kwa mwanamke katika kuwaelimisha kutambua haki zao hususani mfumo dume,pamoja na kuwasaidia watoto yatima,wanaoishi kwa matumaini na mazingira magumu kupata elimu na mahitahi muhimu.

Kikundi cha Ndekira ni moja ya matawi ya kikundi cha akina mama wanaopambana na Ukimwi Mkoani Kilimanjaro(KIWAKUKI)ambacho kinawaunganisha akina mama wa kata 3 za Kibosho Mashariki,Kibosho Kati,na Kata ya Kirima.

Hayo yalibainishwa Mwenyekiti wa Kikundi hicho Catherina Bendict wakati akizungumza na blog hii ambapo amesema katika kutambua hali iliyopo kuhusu mahitaji ya vituo vya maarifa na taarifa ya ukombozi katika ngazi ya jamii vinavyoundwa na mtandao mwaka huu mikoa mbalimbali hapa nchini.

Alisema kuwa kupitia kikundi hicho wakina mama wamekuwa wakipata jukwaa la kudajili mambo mbalimbali yanayowahusu wanawake,ikiwemo kuwasaidia wanawake wengine ambao wamekuwa wakizikosa haki zao kutokana na mfumo dume na kunyimwa na wanaume haki  zao ikiwemo kujiunga kwenye vikundi mbalimbali.

Kwa upande wa watoto yatima na ambao wanaishi kwa matumiani kikundi hicho kinawapatia mahitaji mbalimbali ambapo mpaka sasa kikundi kina watoto yatima wanaosomeshwa na kikundi,na kueleza kuwa tangu mwaka 2004 wametumia zaidi ya million 4 kwa ajili ya mahitaji ya watoto hao.

“Kikundi kilianzishwa mwaka 2004 na mpaka sasa hatuna miradi ambayo inaweza kutuingizia kipato kwa ajili ya kuwahudumia watoto hao,tumekuwa tukifanya sherehe na kualika wageni mbalimbali ambao hutuchangia ambapo kwa sasa ni mradi wa viti ndio tunategema”Alisema Catherina.

Wakielezea changamoto zinazowakabili kwenye warsha hiyo,walisema kuwa kikundi hicho kinakabiliwa na ukosefu wa ofisi kwa sasa ambapo kwa sasa wapo chini ya hospitaki ya Kibosho,pamoja na ukosefu wa fedha kwa ajili ya kuendeshea kazi za ofisi.

“Kikundi chetu kimekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu kwa jamii lakini bado tunahitaji elimu zaidi kwa kujengewa uwezo ili kuweza kuwa mkombozi wa mwanamke na watoto hususani katika maeneo ya vijijini ambayo mfumo dume bado ni tatizo”Alisema.

                                  


No comments:

Post a Comment