Friday, May 25, 2012

WATU WALIOPOTEZA MAISHA KWENYE AJALI YA GARI LA MBUNGE WA ROMBO JOSEPH SELASINI WAONGEZEKA.

Idadi ya Watu waliopoteza maisha kwenye ajali ya gari alilokuwa akiendesha Mbunge wa Rombo Josephy Selasini vimeongezeka na kufika watu wanne baada ya watatu kufariki eneo la tukio huku mmoja akifariki akipatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya KCMC.

Kwa Mujibu wa taarifa kutoka kwa kamanda wa polisi Mkoani Kilimanjaro Absalom Mwakyoma kwa waandishi wa habari alisema kuwa ajali hiyo ilitokea may 24 majira ya saa 19:00 katika barabara kuu ya Moshi kuelekea Arusha eneo la Chuo cha Ufundi Bomango'ombe Wilayani Hai.

Alisema kuwa gari hilo ambalo alikua akiendesha Mwenye ambalo lilikuwa na nambaza usaji T 441 BRT aina ya Toyota Land Cruiser lilikuwa na abiria sita na wanne wameweza kupoteza maisha.

Waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo ni pamoja na mama yake mzazi wa Joseph Selasini Catheriner Roman Selasini(80),Agatha Jerome Mahoo mama mkwe wa Selasini,(85)mkazi wa Rombo ambaye ni mkulima pamoja na wanawake wawili ambao hawajatambulika majina yao mmoja akikadiriwa kuwa na umri wa miaka 70-75 ambaye inasemekana ni pia ni Shangazin wa Joseph Selasini na mwingine mwenye ambaye umri wake unakadiriwa kuwa 35-40.

Majeruhi kwenye ajali hiyo ni pamoja na Mke wa Selasini,Digna Kavishe,(43)ambaye amepata majeraha sehemu za kichwa na hali yake siyo nzuri,pamoja na Joseph Selasini Mwenyewe ambaye amepata majeraha kwenye bega pamoja na mkono wa kulia ila hali yake inaendelea vizuri.

Chanzo cha ajali hiyo kimetajwa kuwa ni mwendokasi pamoja na kupasuka kwa gurudumu la mbele baada ya gari hilo kuingiliwa na pikipiki mbele na kukosa mwelekeo.

Miili ya Marehemu imehifadhiwa kwenye hospitali ya Rufaa ya KCMC kwa ajili ya taratibu za mazishi.

No comments:

Post a Comment