Wednesday, May 16, 2012

Mwenyekiti wa Tume ya Kuratibu maoni juu ya Katiba Jaji Joseph Sinde Warioba(kulia) akizungumza na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati Rais alipomtembelea ofisi kwake jana.Wengine katika picha ni Makamu mwenyekiti wa tume hiyo Jaji mkuu Mstaafu Mhe. Agostino Ramadhani(Watatu kushoto),Waziri wa Katiba na SheriaMhe. Mathias Chikawe(Wapili kushoto) na kushoto ni naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Angela Kairuki

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete jana alitembelea ofisi za Tume ya kukusanya na kuratibu maoni juu ya katiba zilizopo katika jengo jipya katika Wizara ya Mambo ndani jijini Dar es Salaam.Akizungumza na wajumbe wa Tume hiyo Rais Kikwete alirudia ahadi yake ya kuwapatia nyenzo za kazi ikiwemo usafiri ili kuiwezesha tume hiyo kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.Pichani Rais akizungumza na wajumbe wa tume hiyo katika ukumbi wa mikutano uliopo katika jengo la tume hiyo jana.


No comments:

Post a Comment