Sunday, March 10, 2013

USHINDI WA UHURU WAMFUNGA MDOMO MAGUFULI.

Uhuru Kenyetta Rais  wa Taifa la Kenya

WAZIRI wa Ujenzi, Dk John Magufuli jana aliungana na Waziri Mkuu wa Zimbabwe, Morgan Tsavangirai kumpigia debe mgombea wa urais wa Kenya, Raila Odinga huku akisema mgombea huyo kupitia Chama cha Orange Democratic Party (ODM), anastahili kuwa Rais wa nchi hiyo kutokana na sifa zake za uongozi.


Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa ODM jana, Dk Magufuli alisema hakuna sababu zozote zitakazowafanya Wakenya wasimchague Odinga.

“Nataka kuwaambia Wakenya kwamba Odinga ni mcha Mungu, mnatakiwa kujua hilo. Kama mimi ningekuwa Mkenya ningempigia huyu jamaa kura ili aongoze nchi. Lakini sasa kwa kuwa siruhusiwi hata kupiga kura, basi nawaambia msiache kumchagua huyu atawaongozeni vizuri,” alisema Dk Magufuli.


Dk Magufuli alisema kati ya wagombea wote waliojitokeza kuwania kiti cha urais nchini Kenya, hakuna anayemfikia Odinga na hiyo inaonyesha kuwa wakimchagua atawasaidia bila ubaguzi.

Waziri Dkt Magufuli.
Alisema na hata Odinga ambaye ni Waziri Mkuu wa Kenya akiamua kugombea ubunge katika Jimbo lake la Chato, hawezi kumshinda.
“Kwa hiyo nasimama hapa ndugu zangu wana ODM kuwapa pongezi kubwa sana, mmmefanya kitu kikubwa sana kwa sababu mmechagua jembe,” alisema.

No comments:

Post a Comment