Tuesday, February 19, 2013

MTOTO ALIYENUSURIKA KIFO BAADA YA NYUMBA ALIYOKUWA KUTEKETEA KWA MOTO.


 Mtoto Ombeni Mbeula ambae ameungua kwa moto vibaya kama anavyoonekana anahitaji msaada  wako.Wadau samahani kwa picha hizi

 

                                      Mama wa mtosto Kilaudia Kigailaakiwa na mwanae huyo.
HUJAFA hujaumbika bado mtoto Ombeni Mbeula amenusurika kifo baada ya nyumba aliyokuwa akiishi kuteketea kwa moto  wakati mtoto huyo akiwa ndani baada ya mama wa  mtoto huyo kuwaacha watoto hao na kwenda shamba eneo  Chitemo wilaya ya mpwapwa mkoani Dodoma.
Imedaiwa kuwa moto huo ulitokea wakati mvua inanyesha ghafla nyumba ilibomoka na wakati huohuo walikuwa watoto wawili walikuwa jikoni ndani ya hiyo nyumba na ndipo  kijana huyo alipotetekea kwa moto
Baada ya tukio hilo kutokea   ikafanyika uokoaji kwenye nyumba hiyo maeneo ya Chitemo na kufanikisha   kuokoa watoto wote wawili kati ya mmoja aliumia kwa kuangukiwa na udongo wa nyumba hiyo na huyu Ombeni Mbeula aliangukia kwenye moto mpaka kuungua hivi unavyoona kwenye picha lakin hali zao ni salama kwa wote.
Baada ya uokoaji waliamua kumpeleka mtoto huyo kwenye hospitali ya Mima iliyoko Mpwapwa ikashindikana madaktari wakamuagiza aende hospitali ya Mpwapwa hapo hospitalini wakakaa siku mbili katika hospitali ya mpwapwa  na siku ya tatu wakaambiwa waende hospitali ya rufaa iliyoko Dodoma Mjini ambayo ni inajulikana General kwa matibabu zaidi.
Walipofika katika hospitali ya mkoa wa Dodoma wakaanza matibabu lakini uwezo wa kipato cha wazazi wake sio kizuri inahitajika msaada kwa matibabu maana hata dawa hajapatiwa na pesa kwa ajili ya matibabu  haikuweza kupatikana paka sasa
Kama umeguswa kutoa ni moyo sio utajiri muokoe mtoto huyu maana hata kula anashindwa mpaka kuona anaona kwa mbali sana.
Mama yake hana simu lakini anatumia simu ya  ndugu yake Ekiria Paskali
Kwa yeyote atakayependa kumchangia mtoto huyo atume chochote kwenye namba hii au atumie M- pesa kwenye namba hii 0757 498336
PICHA KWA HISANI YA PAMOJAPURE BLOG

No comments:

Post a Comment