Thursday, December 20, 2012

MAKAMU WA RAISI DK BILAL AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI.

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi katika Ujenzi wa Nyumba za Makazi ya Watumishi wa Umma, zilizopo eneo la Ada Estate, jijini Dar es Salaam, leo Desemba 20, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, na Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli, kwa pamoja wakifunua kitambaa kuashiri uwekaji wa Jiwe la Msingi katika Ujenzi wa Nyumba za Makazi ya Watumishi wa Umma, zilizopo eneo la Ada Estate, jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Elius Mwakalinga, wakati akitembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa Nyumba za Makazi ya Watumishi wa Umma, zilizopo eneo la Ada Estate, jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi katika Ujenzi wa jengo hilo leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo na kuonyeshwa Ramani ya Jengo na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Elius Mwakalinga, wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi katika Ujenzi wa Nyumba za Makazi ya Watumishi wa Umma, zilizopo eneo la Ada Estate, jijini Dar es Salaam, leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi ya sanamu la Kinyago cha Umoja, kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Elius Mwakalinga (kulia) na Mwenyekiti wake, Edward Ngwalle, (wa pili kulia) wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi katika Ujenzi wa Nyumba za Makazi ya Watumishi wa Umma, zilizopo eneo la Ada Estate, jijini Dar es Salaam, leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika Picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa TBA, baada ya hafla hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli, wakati akiondoka eneo la Ada Estate, baada ya kuweka Jiwe la Msingi katika Ujenzi wa Nyumba za Makazi ya Watumishi wa Umma, zilizopo eneo la Ada Estate, jijini Dar es Salaam, leo.

No comments:

Post a Comment