Tuesday, November 13, 2012

KAMPUNI YA SIMU ZA MKONONI TIGO KUTOA VIFAA VYA NISHATI YA JUA KWA AJILI YA KUCHAJIA SIMU

Meneja mradi wa kampuni ya simu Tigo Bw.Yaya N’djore (katikati) akiongea na waandishi wa habari  kuhusu kuwapatia wateja wa tigo vifaa vya nishati ya jua (SOLA)wanaoishi mbali na vyanzo vya umeme wateja watakao faidika na huduma hiyo ni wale wanaomiliki maduka ya tigo pesa vifaa hivyo vitakuwa vinapatikana kwenye maduka ya tigo kwa bei ya shilingi 50,000(kushoto)Afisa Masoko wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Jacqueline Nnunduma(kulia)Afisa mahusiano msaidizi kampuni ya simu ya tigo Bi.Mariamu Mlangwa, mkutano huo ulifanyika kwenye Hotel ya southern sun jijini Dar es Salaam
Baadhi ya waandishi wa habari waliodhuria katiaka mkutano huo

Balozi wa kinywaji cha Hennessy kukutana na wafanyabiashara

Balozi wa kinywaji cha Hennessy Cyrile Gautier Auriol,  akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusiana na mikakati yake ya kufanya mazungumza na wafanya biashara mbali mbali wa hapa nchini.  Picha/ Mpiga Picha Wetu)
……………………………
Na Mwandishi wetu
Balozi wa kinywaji cha Hennessy, Cyrile Gautier Auriol, yupo nchini kwa ajili ya shughuli mbali mbali pamoja na kukutana na wafanyabiashara wa jiji la Dar es Salaam.
 
Auriol aliwasili jijini leo na kufanya mazungumza na wenyeji wake kabla ya kuelezea nia ya safari yake ambayo lengo kubwa ni kutanua soko la kinywaji hicho maarufu duniani kwa Watanzania nan chi za Afrika Mashariki.
 
Alisema kuwa pamoja na kukutana na wafanyabiashara, pia atakutana na watu wa sekta tofauti, miongoni mwao ni wanamuziki na wanamitindo.  Ziara ya balozi huyo itakuwa ya siku tano.
 
Alifafanua kuwa ujio wake ni mara ya pili kwa ukanda wa Afrika Mashariki na ameona kuna mafanikio makubwa kwa wafanyabiashara na hasa katika soko la vinywaji vikali.
 
Alisema kuwa kinywaji cha Hennessy kwa sasa ndicho kinatamba katika ukanda huu na hivyo kuna haja kwa Watanzania  kuanza kupartavradha kwa ajili ya kujenga mwili na afya bora. Ikiwa na zaidi ya historia ya miaka 250, Hennessy inatajwa kuwa kinywaji (Cognac) bora zaidi duniani.
 
Pia Auriol atakutana na wapenzi wa Hennessy katika matukio mbalimbali maalumu ikiwemo chakula cha mchana katika hoteli ya Hyatt Regency ambapo baadhi ya wanawake watakaochaguliwa watapata fursa ya kujifunza historia ya kinywaji cha Hennessy lakini pia kuonja aina mbalimbali za kinywaji hicho lengo likiwa kuwafundisha wanawake namna ya kufurahia kinywaji hicho wakiwa majumbani mwao.
 
Balozi Auriol pia atahudhuria chakula cha jioni na wafanyabiashara wa hapa nchini katika mgahawa wa Akemi uliopo katika ghorofa la Diamond Jubilee. Balozi Auriol atatoa elimu kuhusu Hennessy ikifuatiwa na uonjaji wa kinywaji hicho pamoja na chakula kitakachoandaliwa na mpishi mkuu wa hotel hiyo.
 
Ziara ya balozi Auriol inaenda sambamba na juhudi nyingine za kutangaza kinywaji hicho hapa nchini, mojawapo ikiwa ni kampeni ya mabango ya ‘Flaunt Your Taste’ yaliyosambaa jiji zima pamoja na ukamilishaji wa chumba cha Hennessy kilicho katika Club 327, ambacho balozi Auriol atakizindua.
 
Balozi Auriol atakuwa na kikao maalumu pia na wapenzi wakubwa wa kinywaji hicho, na pia atawazawadia mialiko maalumu ya kuingia kwenye klabu ya wapenzi wa kinywaji hicho ya Afrika mashariki.
 
Pia atatoa mafunzo maalumu kwa baadhi ya wahudumu kutoka katika bar kubwa za jijini. Lengo kuu la mafunzo hayo yatakayofanyika katika hoteli ya Southern Sun na George & Dragon ni kuwapa wahudumu ujuzi utakaowawezesha kutoa huduma bora na ya kipekee kwa wateja wao wakati wakiburudika na kinywaji cha Hennessy kwenye bar au hotel wanazozipendelea.

Matukio ya uchaguzi wa CCM mjini Dodoma leo

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete  akizungumza katika Mkutano mkuu wa CCM kwenye ukumbi wa Kizota Mjini Dodoma Novemba 13, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakauya Kikwete akipiga kura katika mkutano mkuu wa CCM kwenye mkutano mkuu wa CCM kwenye ukumbi wa Kizota mjini Dodoma leo)
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, Makamu Mwenyekiti wa CCM (bara)) Phili Mangula (katikati) na Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM,Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakifurahia jambo katika Mkutano Mkuu wa CCM uliomalizika  Novemba 13, kwenye ukumbiwa Kizota Mjini Dodoma . (Picha na Ofisi ya Waziri mkuu)


KARAOKE NIGHTS AT MBALAMWEZI BEACH CLUB


GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ SEASON 2 KEY MESSAGES – EA

The GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™, the TV game show phenomenon which has excited audiences across Africa for the last two years, is back for an incredible 2nd Season, and this time around, it’s going to be Pan-African!
 Guinness® is calling upon football fans to play for their country in the new Pan-African show, as contestants from Kenya, Tanzania, Uganda, Cameroun and Ghana go head-to-head
 Successful teams could win up to 900,000 USD in Season 2, as contestants represent their nation to find out who is Made of More and has the skill and knowledge to go all the way and be crowned Pan-African champions
 In the new Season even more people can get involved in the GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ in a number of different ways.  Alongside the exciting new TV show there will be the return of the GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ mobile phone game so that fans can test their football trivia on their mobile phone; and live GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ quizzes in bars
 AUDITION EVENTS
Guinness® is searching for football lovers who have what it takes to represent Tanzania on a Pan-African stage, and show that they can achieve their potential and be recognised as players, rather than spectators in life
 Players can try out for a chance to appear in the show at the GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ audition events.  Three events to search for the stars of Season 2 of the GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ will be held in:
At Leaders Club, Dar es Salaam on 24th November
 Teams of two football fans who think they have the brains and the brawn to step up and represent Tanzania in the GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ should come along and try out for the show.  One of you will need to demonstrate great skill with a ball at your feet, and your partner should know everything there is to know about the beautiful game. You will be put through your paces in a series of challenges to see if you could represent your nation and be in with a chance of winning up to 900,000 USD.
 The GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ audition events will be a fun day out for everyone, with football activities, music and entertainment. Entry is free but will be restricted to only those 18+. 

WADAU ZANZIBAR WAOMBWA KUCHANGIA SHULE ZA KATA TEMEKE DSM

Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya ‘Cooperation for assisting handicapped people’ inayojishughulisha na kusaidia watu wasiojiweza Mhina Michael Shengena akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Rahaleo Mjini Zanzibar kulia yake ni Mhariri Mkuu wa Maelezo Fakih Haji Mbarouk.
 (Imetolewa na Idara ya Habari Maelezo Zanzibar)
 …………………………………………….
Na Mwanaisha Mohammed-Maelezo Zanzibar                      

Wadau na Makampuni mbali mbali Zanzibar wameombwa kuichangia Taasisi ya ‘Cooperation for assisting handicapped people’ inayojishughulisha na kusaidia watu wasiojiweza ili Taasisi hiyo iweze kujenga Mabweni ya Shule mbili za kata Temeke Jijini Dar es Salaam.
 Ombi hilo limetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni hiyo Mhina Michael Shengena wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Rahaleo Mjini Zanzibar.
 Amesema wanahitaji wasaidiwe Sh Milioni Arobaini (40,000,000) ndani na nje ya Zanzibar kwa ajili ya ujenzi wa Mabweni ya watoto Yatima,Walemavu na Watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi ili waweze kupata taaluma ambayo itawasaidia katika maisha yao.
 Amezitaja Shule ambazo wana mpango wa kujenga mabweni kwa wanafunzi hao kuwa ni Nguva na Sumangira zilizopo katika Manispaa ya Temeke Jijini Dar es Salaam.
 Aidha ametaja njia ambayo Wadau mbalimbali wanaweza kuchangia msaada wao kwa Kampuni hiyo kufanikisha ujenzi huo kuwa ni kupitia akauti namba 01J2070153800 ya CRDB Bank.
 Mkurugenzi Mhina ameongeza kuwa watakuwa na ziara ya nchi nzima ambapo wanatarajia kukutana na Viongozi wa Serikali, Siasa, Dini na Wananchi mbali mbali katika kuitangaza Taasisi yao ili wadau waweze kuifahamu na kuichangia.
  Aidha ametoa wito wa wananchi wa Zanzibar kushiriki katika harambee ya kuichangia Taasisi yao itakayofanyika Ukumbi wa Hoteli ya Bwawani January 30, mwaka 2013 mjini Zanzibar.
 Taasisi ya ‘Cooperation for assisting handicapped people’ yenye Makao Makuu yake Mkoani Iringa imesajiliwa mwaka 1998 chini ya Sheria za makampuni ya Tanzania Bara na kupewa namba za usajili 3388 ambapo shughuli yake kuu ni kusaidia watu wasiojiweza.
habari picha na bukuku blog.

No comments:

Post a Comment