NAIBU SPIKA ATAKA VYOMBO VYA HABARI VISIWAONEE HURUMA VIONGOZI MAFISADI
Ndungai ambaye ndie alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya kitaifa ya siku ya Uhuru wa vyombo vya habari duniani alitoa kauli hiyo Leo katika ukumbi wa Mlimani City jijini D'salaam wakati akiwahutubia wanahabari katika Sherehe zilzoandaliwa na Misa Tanzania na mfuko wa vyombo vya habari Tanzania ( TMF) .
Alisema kuwa wakati wanahabari nchini
wanaadhimisha siku ya Uhuru wa vyombo vya habari ni vema wanahabari
kuendelea kutathimini mwenendo mzima wa uwajibikaji katika kuandika
habari za wale wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Kwani alisema kuwa pamoja na jitihada mbali mbali vinazofanywa na vyombo vya habari katika kuandika habari za kifisadi ila bado nguvu kubwa inatumika kuwafichua viongozi mafisadi waliopo madarakani na kuwaonea huruma viongozi wajao jambo ambalo ni hatari zaidi .
Alisema kinachotokea leo kwa vyombo vya habari kuandika habari za mafisadi wa sasa waliopo madarakani na kuwaonea huruma viongozi wajao bila kuwasema ni kutolitendea haki Taifa na siku watakaoingia madarakani nchi itayumba zaidi.
Hata hivyo alisema kuwa juhudi za wanahabari na vyombo vya habari nchini katika kuhabarisha umma zimeendelea kuwa kubwa zaidi na kuwa hata shughuli za bunge zimekuwa zikiwafikia wananchi kutokana na ushirikiano mzuri uliopo Kati ya bunge na wanahabari.
"kweli uwajibikaji wa vyombo vya habari kwa sasa ndio umepelekea hata kasi ya wananchi kufuatilia vikao vya bunge kuongezeka zaidi na hata wabunge kuchangia bungeni kuongezeka japo wanahabari mmekuwa mkituchapa sana ....Kwani mara kwa mara mmekuwa mkipiga picha wabunge wanaosinzia japo sisi wabunge hatusemi Kusinzia tunakuwa tunatafakari ......ila nasema kazi nzuri sana mmekuwa mkiifanya" alisema Ndungai
Katika hatua nyingine naibu spika huyo aliahidi kuwa bunge litaendelea na ushirikiano na vyombo vya habari na kuwa hata miswaada miwili itakayofikishwa bungeni juu ya mapendekezo ya Uhuru wa vyombo via habari Pindi itakavyofikishwa bungeni
Kwani alisema kuwa pamoja na jitihada mbali mbali vinazofanywa na vyombo vya habari katika kuandika habari za kifisadi ila bado nguvu kubwa inatumika kuwafichua viongozi mafisadi waliopo madarakani na kuwaonea huruma viongozi wajao jambo ambalo ni hatari zaidi .
Alisema kinachotokea leo kwa vyombo vya habari kuandika habari za mafisadi wa sasa waliopo madarakani na kuwaonea huruma viongozi wajao bila kuwasema ni kutolitendea haki Taifa na siku watakaoingia madarakani nchi itayumba zaidi.
Hata hivyo alisema kuwa juhudi za wanahabari na vyombo vya habari nchini katika kuhabarisha umma zimeendelea kuwa kubwa zaidi na kuwa hata shughuli za bunge zimekuwa zikiwafikia wananchi kutokana na ushirikiano mzuri uliopo Kati ya bunge na wanahabari.
"kweli uwajibikaji wa vyombo vya habari kwa sasa ndio umepelekea hata kasi ya wananchi kufuatilia vikao vya bunge kuongezeka zaidi na hata wabunge kuchangia bungeni kuongezeka japo wanahabari mmekuwa mkituchapa sana ....Kwani mara kwa mara mmekuwa mkipiga picha wabunge wanaosinzia japo sisi wabunge hatusemi Kusinzia tunakuwa tunatafakari ......ila nasema kazi nzuri sana mmekuwa mkiifanya" alisema Ndungai
Katika hatua nyingine naibu spika huyo aliahidi kuwa bunge litaendelea na ushirikiano na vyombo vya habari na kuwa hata miswaada miwili itakayofikishwa bungeni juu ya mapendekezo ya Uhuru wa vyombo via habari Pindi itakavyofikishwa bungeni
No comments:
Post a Comment