Thursday, May 3, 2012


 Chama cha waandishi wa habari Mkoani Kilimanjaro(MECKI)kimeadhimisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari kwa kujitolea kwenye shughuli za kijamii.

Makamu Katibu Mkuu wa Chama cha waandishi mkoani Kilimanjaro(kulia)Nakajumo James akikabidhi msaada wa unga wa ngano kwa Mkurugenzi msaidizi wa kituo hicho bw Elisonguo Benjamen Kiwelu   ikiwa ni sehemu ya msaada ukiotolwa kwa siku ya uhuru wa vyombo vya habari,kushoto ni Mwekahazina wa chama hicho Jane Mhalila.


Waandishi wa habari ambao ni wanachama wa chama cha wanahabari Mkoani Kilimankaro(MECKI)wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kufika kwenye kituo cha watoto yatima cha treasures of afrika childrens home kilichopo shanti town manispaa ya moshi
Watoto wanaolelewa na kituo cha  treasures of afrika childrens home wakiwasikiliza waandishi wa habari hawapo pichani

WAANDISHI WA HABARI NA WANACHAMA WA PRESS CLUB YA KILIMANJARO WAKIWASIKILIZA MKURUGENZI MSAIDIZI WA KITUO CHA treasures of afrika childrens homE(hayupo pichani )
Picha ya pamoja kati ya waandishi,watoto wanaoishi kwenye kituo cha treasures of afrika childrens home
Salome Kitomary ambaye ni mwandishi wa habari wa magazeti ya Nipashe na The Gurdian ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati tendaji wa Chama cha waandishiakiwa kwenye zoezi la kupanda miti kama sehemu ya kuadhimisha siku ya vyombo vyua habari.

Hapa ni Mwandishi wa habari wa gazeti la Habari Leo Arnold swai akipanda mti wake kama sehemu ya kuazimisha siku ya vyombo vya habari.
                                                                           
Chama cha waandishi wa habari Mkoani Kilimanjaro(MECKI)kimeeadhimisha siku ya uhuru wa habari kwa kujitolea kwenye shughuli za kijamii ikiwemo kutoa msaada wa vyakula,vinywaji mafuta na sabuni kwa kituo cha watoto  yatima cha treasures of afrika childrens home  pamoja na kupanda miti katika manispaa ya moshi.

Akizungunza wakati wa ziara hiyo Kaimu katibu Mkuu wa Chama cha waandishi Mkoani hapa Nakajumo James amesema kuwa chama hicho kimeamua kufanya hivyo kama njia pekee ya kuwafanya watoto hao wanaoishi kwenye kituo hicho wasione wametengwa na jamii.

Amesema kuwa waandishi wamekuwa wakiandika habari za watu na taasisi mbalimbali ambao wamekuwa wakijitoa kwenye shughuli hizo,hivyo ni vyema wakaitumia siku ya vyombo vya habari dunia nao kusaidia watoto yatima pamoja na watu walio na mahitaji maalumu.

Akizungunmza kwa niaba ya Makamu Mwenyekiti wa Mecki Mtunza hazina wa chama hicho Jane Mhalila amegusia malezi wanayopatiwa watoto kuwa ni mazuri na yanaendana na wakati kwa kuzingatia hali halisi ya madaliko ya kisayansi na teknolojia,na kupata huduma ya kiroho.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa kituo hicho bw Elisonguo Benjamen Kiwelu amesema kuwa kituo hicho kina watoto wapatao 26 wanaosoma shule za msingi na sekondari ambao wanakuwa tayari wamedhibitishwa na ustawi wa jamii kuwa hawana msaada wowote.

Hata hivyo ameseme akuwa kituo hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kupanda kwa garama za maisha,unaotokana na mfumuko wa bei ya vitu wanavyohitaji wattoo hao.

Kituo  cha Treasures of Afrikan   Children home  kilianzishwa mwaka 2006 na kuanza kuchukua motto wa kwanza mwaka 2007 na hadi sasa kina watto wapatao 26 na wafanyakazi waangalizi 20.

No comments:

Post a Comment