Tuesday, March 20, 2012

MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI YAKIWA YAMEFIKIA KILELE HIVI KARIBUNI WANANCHI WILAYANI MWANGA WAMELALAMIKIA UPATIKANAJI WA HUDUMA YA MAJI SAFI NA SALAMA PAMOJA NA HUDUMA YA AFYA
Miongoni mwa miradi iliyokwama kukamishwa ya  kituo cha afya cha kileo ambacho hadi sasa huduma zake zinasua sua,hivyo kulazimu wakiana mama wajawazito kufika hadi hospitali ya mkoa ya mawenzi kwa ajili ya matibabu na kujifungua,kituo kipo ila hakina dawa wala wahudumu,

Wananchi wa kijiji hicho wanasema kuwa Mbunge wa Jimbo hilo Jumanne Magembe aliahidi kuwepo kwa huduma stahiki ya afya kwenye kituo hicho wakati wa kampeni lakini baada ya kuchaguliwa hawajawahi kufika kijijini hapo.

Wanasema kuwa kituo hicho ni jengo tu na maandashi lakini hakuna huduma yoyote,hata kama mgonjwa kama anahitaji huduma ya kwanza wahudumu wa afya ,hawapatikani hususani nyakati za usiku. 
 
Wananchi wa kijiji cha Kileo kilichopo Kata ya Kileo Wilayani Mwanga wakizungumza keo mbalimbali zinazokabili eneo hilo ikiwemo lile la maji pamoja na miundombinu yake
Bakari Mmbaga akizungumzia shughuli mbalimbali za maendelo kukwama kutokana na kutokuwepo kwa ushirikiano baina ya  wananchi na viongozi ngazi ya kijiji na Kata.


Hali ya upatikanaji wa maji kidogo ni shida na wanafunzi na wakina mama ndio waadhirika wakubwa katika suala zima la kutafuta huduma hiyo
 

No comments:

Post a Comment