RC KILIMANJARO AVIKALIA KOONI VIWANDA VINAVYOTUMIA MAGOGO KILIMANJARO.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro
Leonidas Gama amepiga marufuku viwanda vyote vinavyotumia magogo mkoani hapa,
kutoingia mkataba wa uvunaji miti na watu wasiokuwa na mashamba, na badala yake
amevitaka kilima mashamba yao
wenyewe ili viweze kujiendesha.
Gama aliyasema hayo jana wakati
wa operesheni ya siku kumi ya kupanda
miti 29,000 katika eneo la ukanda wa hafu maili lililopo wilaya ya Moshi
vijijini, ambapo alisema kuwa wamiliki wa viwanda vinavyotumia magogo wamekuwa
wakiingia mikataba na watu wasikuwa na mashaamba ambao huwapeleka kuvuna miti
ya asili kwenye msitu wa mlima Kilimanjaro.
Alisema kuwa viwanda hivyo
vinapaswa kulima mashamba yao
ya kuvuna magogo na sio kufanya uharibifu kwenye misti ya asili, hali aliyosema inapelekea mkoa wa Kilimanjaro
kuwa jangwa.
Gama alivitaka viwanda hivyo
kuingia mikataba kwenye misitu ya serikali nasio kuvuna miti kiholela, na
kuzitaka halimashauri zote kusimamia sheria za misitu kikamilifu lengo likiwa
ni kurudisha misti yote ya asili inayozunguka milima na barafu yake.
Alisema kuwa kwasasa ukame uliopo mkoani hapa unatishia uhai wa
wananchi, kutokana na mito
na chemu Chemu iliyokuwa ikitiririsha maji toka mlimani kukauka sababu zikiwa
ni kilimo kandokando ya vyanzo vya maji, ukataji miti ovyo pamoja na uchomaji
mioto.
Gama alisema kuwa lazima kila
halimashauri iwajibike kuhakikisha inasimamia sheria za misitu, ikiwa ni pamoja
na kudhibiti mifugo ambayo faini yake
alisistiza iwe kubwa kuliko bei ya mfugo wenyewe, pamoja na kutoa zawadi kwa mtu
atakaetoa taarifa za mashine ya kuvuna miti “chensoo”.
Tunanata tufikie lengo la
kerejesha uoto wa awali, hivyo halimashauri zitatoa shilingi 50,000 kwa mtu
atakae toa taarifa ya kutumika kwa mashene ya kuangusha miti “Chensoo” pia
zitaoa shilingi 50,000 kwa mtu atakaeonyesha sehemu mti ulipokatwa siku hiyo na
kudhibitishwa” alisema Gama.
Gama alisema kwa ukanda huo jana
walifanikiwa kupanda miti 2,100 ambapo katika eneo hilo lengo ni kupanda miti
29,000 na kueleza kuwa katika operesheni hiyo ya siku kumi lengo ni kuhakikisha
wanapanda miti milioni 8.2 kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali, mashule,
hosptali na mtu mmoja mmoja.
No comments:
Post a Comment