UZINDUZI WA KAMPENI YA KUPANDA MITI YAENDELEA MANISPAA YA MOSHI MKOANI KILIMANJARO

Hapa Mkuu wa Mkoa Leonidas Gama akizindua zoezi hilo kwa kupanda mti katika eneo lijulikanalo kwa jina maarufu la Changbuy na kuendelea kupanda katika maeneo mengine.
Hapa Mkuu wa Mkoa Leonidas Gama akizindua zoezi hilo kwa kupanda mti katika eneo lijulikanalo kwa jina maarufu la Changbuy na kuendelea kupanda katika maeneo mengine.
Mdau kutoka bank ya standard chartered akipada mti kwenye zoezi hilo la upandajiw a miti |
Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Bernadette Kinabo naye akipanda mti kwenye zoezi hilo la upandaji wa mti kwenye Manispaa ya Moshi. |
Meya wa Manispaa ya Moshi Japhary Michael(Chadema)akipanda mti wake eneo la Meimorial |
Wadau Mbalimbali waliohudhuria zoezi hilo la uzinduzi wa kampeni za upandaji wa mti. |
Akizungumza kwenye uzunduzi wa kampeni hizo za upandaji wa
miti Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama amesema kuwa zeozi hilo litakuwa endelevu na uongozi wa mkoa
utahakikisha kuwa kila miti ambayo itakuwa unaoteshwea na halmashauri zote za
Mkoa wa Kilimanjar inatunzwa na kukua na
siyo kutekelezwa.
Mkuu huyo amesema kuwa katika utaratibu huo ulioanzishwa wa
upandaji wa miti Mkoa wa Kili,manjaro utatarajia kupanda miti zaidi ya million
50 baada ya miaka mitano.
Amesema kuwa katika kipindi hiki cha operesheni ya upandaji
wa miti wanatarajia kupanda miti zaidi ya million nane.
Amesema kuwa zoezi hilo litakuwa endelevu na ni suala la
watu wote kuhakiklisha kuwa wanasimamia mazingira ipasavyo,huku akisifu wilaya
za moshi Mjini na Hai katika utunzania wa
mazingira.
Alisema kuwa upandaji huo wa miti utazingatia maeneo makuu manne
katika utunzaji wa mazingira kama kingo za mito,vyanzo vya maji,chemchem,milima
na maeneo hayo yatatakiwa kutambuliwa na halmashauri ili kuweza
kusimamiwa ipasavyo.
"Taaisisi mbalimbali zijitokeza kusaidia halmashauri
zetu ili kuweza kifanikisha mpango huu,lakini pia kwa mwaka 2013 lazima kila
kijiji kuanzisha vitalu vya miti pamoja na watu binafsi na sisi tutakachofanya
ni kuwasaidia upatikanaji wa miche"Alisema Gama
Hata hivyo aliwashukia wafugaji ambao wamekuwa wakiacha
mifugo yao kuzagaa ovyo,huku akiwataka watendaji wa Serikali kutoza faini kubwa
zaidi kwa mifugo ambayo itakamatwa ikiharibu mazingira ili kuweza kutokomeza
kabisa tatizo hilo.
No comments:
Post a Comment