PICHA NA MATOKEO YA UCHAGUZI ARUMERU.
![]() |
NAWASHURU SANA WANA ARUMERU KWA KUNICHAGUA NI KAULI YAKE JOSHUA NASARI MAENEO YA ELEPHANT HOTEL ARUMERU LEO ASUBUHI |
TUMEFURAHI JAMANI,CHADEMA IMEPITA WANANCHI WA ARUMERU WAKIMSIKILIZA MSHINDI JOSHUA NASARI.
Mbunge mteule wa Arumeru Mashariki Mh. Joshua Nasari akiongea
baada ya kutangazwa kuwa mshindi asubuhi hii huko Arumeru
Mbunge mteule wa Arumeru Mashariki Mh. Joshua Nasari akiongea
baada ya kutangazwa kuwa mshindi asubuhi hii huko Arumeru
Matokeo
ya kura za Ubunge jimbo la Arumeru Mashariki yametangazwa sasa hivi na
Msimamizi wa Uchaguzi na Mkurugenzi wa Wilaya ya Arumeru Bw Gracias
Kagenzi amemtangaza mgombea wa CHADEMA Bw Joshua Nassari kuwa mshindi
baada ya kupata kura 32,972 dhidi ya mpinzani wake wa karibu kutoka CCM
Bw Sioi Sumari aliyepata kura 26,757
Matokeo kwa Vyama vingine sita vilivyoshiriki ni kama ifuatavyo
DP -77
NRA - 35
AFP - 139
UPDB - 18
TLP - 18
SAU - 22
Kwa
mujibu wa Bw Kagenzi zaidi ya watu 120,000 walijiandikisha na
aliojitokeza na kupiga kura walikuwa 60,696 ambapo kura halali zilikuwa
60,038 na zilizoharibika ni kura 661.
Wakati
huo huo, habari kutoka Mwanza zinasema CHADEMA
kimeshinda katika uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kirumba
mkoani Mwanza.
Msimamizi wa uchaguzi huo,
Bw. Aloyce Mkono, amemtangaza kuwa mshindi mgombea wa Chadema Mh Dany
Kahungu kwa kura 2,938 dhidi ya mgombea wa CCM Mh Jackson Masamaki
aaliyepata kura 2,131.
Wagombea wengine walioshindwa vibaya
katika uchaguzi ni pamoja na Mh Haji Issa wa CUF aliyepata kura 184,
Mh Kasala Muhana wa UDP amepata kura 7 na Mh Athuman Jumanne wa NCCR
Mageuzi aliyeambulia 0 katika uchaguzi huo .
Msimamizi huyo alisema kuwa
uchaguzi huo umefanyika katika hali ya amani
na utulivu,na kuwashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi katika
uchaguzi huo na kuonyesha utulivu mkubwa wakati wa uchaguzi na zoezi
la kutangazwa kwa matokeo.
No comments:
Post a Comment