Tuesday, April 17, 2012

MWANANCHI AOMBA MSAADA WA KISHERIA BAADA YA KUDHULIMIWA SHAMBA NA WENYE UWEZO WA KIFEDHA.
Mkazi wa Old Moshi ambaye anajishughulisha na kilimo Shedrack Lyatuu (53) ameiomba Serikali kuingilia kati dhuluma ya kunyanganywa  shamba lake lenye ukubwa wa hekari nne lililopo kijiji cha Sango kwa kuuzwa kwa mfanyabiashara John Mwase kinyume na makubaliano yake.

Akizungumza na waandishi wa habari Shedraki alisema kuwa shauri hilo tayari lilikwishapelekwa mahakamani likiwa shauri namba 56 la mwaka 2011 kwenye mahakama ya moshi wahusika wakiwa ni Shedrack Lyatuu na Henry Samky.

Shedrack alisema kuwa alikabidhiwa eneo hilo ambalo ni la uridhi  febriari 6 mwaka 2007 na kusema kuwa baada ya kukabidhiwa alifanya shughuli za kilimo mwaka 2010 na wakati akiendelea kulima ndipo alianza kukuta mambo ya ajabu ambayo yanamahusiano na ushirikikana.

Alisema kuwa mwaka mwaka 2011wakati akijiandaa na kilimo alikuta mawe yameweka shambani na akaendelea kulima ndipo aliripoti polisi Mhusika akafika na kusema ameuziwa shamba na Henry Samky.

“Nilifika shamabani kwa ajili ya kilimo  walivyonikuta wakanikamata na kunipeleka polisi mwaka 2011 ilikuwa January,na kesi ikafunguliwa kwa kumzuia kumzuia mhusika asifanye shughuli za ujenzi kwenye shamba lake licha ya kwamba mimi nlikuwa sijauza shama langu”Alisema Lyatuu.

Alisema kuwa Henry Samky ambaye ndiye aliyemuuzia Ambrose Mwase mkataba aliouonesha hakua halali kutokana na kuonesha kuwa alimuuzia shamba hili mwaka 1990 wakati shamba hilo alikabidhiwa mwaka 2007.

Hata hivyo alisema kuwa licha ya hukumu ya kesi iliyokuwa mahakamanu ambayo ilitolewa hukumu mwaka jana mwezi wa 12 hukumu hiyo haiokuwa ya haki kutoka na Shedrack kuonekana kama yeye ndiye aliyekuwa analalamikiwa lakini kutokana na kukosa uwezo wa uelewa wa kisheria amekosa la kufanya.

Mimi nilisafiri kwenda mbeya desemba 1984  na na kurudi nyumbani mwaka 2006 na mwaka februari 6 mwaka 2007 nikakabidhiwa shamba la uridhi mimi na kaka yangupamoja na wazee wa mila sasa nashangaa huo mkataba wa kuuza shamba mwaka 1990 nilisaini lini”Alilalamika Shedrack.

Kwa upande wa Mfanyabiashara anayelalamikiwa kununua shamba hilo John Ambrose Mwase alisema kuwa shamba hilo alinunua kwa Henry Samky baada kumhakikishia kuwa shamba hilo ni lake na kumuonyesha mkataba alionunua kwa mmiliki wa shamba hilo ambaye ni  Shedrack Lyatuu.


No comments:

Post a Comment