Friday, April 13, 2012

Diwani wa Kata ya Hai Mjini Japhary Kiure naye aanza harakati za upandaji wa miti.

Diwani wa Kata ya Hai Mjini(kulia)Japhary Michael akipanda mti katika eneo la kingereka lililopo wilayani Hai



Wakina mama nao hawakuwa nyuma kwenye zoezi hilo.

Diwani wa Kata ya Hai Mjini (Chadema)Japhary Kiure leo amepanda miti zaidi ya 100 kwenye mlima wa kingereka uliopo kwenye kata hiyo Wilayani Hai kwa lengo la kuendeleza harakati za upandaji wa miti na kuboresha mazingira.

Akizungumza  wakati wa kupanda miti hiyo Bw Kiure amesema kuwa mkakati aliojiwekea baada ya kuzindua upandaji huo wa miti leo ni kupanda miti maeneo mbalimbali ikiwemo milima,vyanzo vya maji na maeneo ya makazi ya watu.

Amesema kuwa zoezi hilo la upandaji wa miti amelifanya kuitikia wito wa kitaifa wa upandaji wa ambapo katika eneo aliliopanda miti la mlima wa kingereka ulikuwa tayari umekwishaanza kuadhiriwa na mmonyoko wa udongo kutokana na kukosa miti na kuharibiwa na mifugo.

Kiure amesema kuwa katika kuweka mikakati ya kufanikiwa kwenye zoezi hilo amekwisha hamasisha waannchi kupitia kwenye vikao mbalimbali na kutaka kila kaya kupanda miti zaidi ya kumi pamoja na kujitolea miti kwenye  taasisi kama mashule.

Amesem kuwa baada ya kupanda miti 100 aliyoipanda kama uzinduzi,matarajio yake ni kupanda miti zaidi ya 5000 katika kipindi chake cha uongozi ambayo atahakikisha inasimamiwa na kutunzwa ili isikauke na kuweka utaratibu mzuri wa kudhibiti mifugo ambayo imekuwa ikiharibu miti hiyo.

Kwa upande awake Abibu adam lema ambaye ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Kingereka amewataka wafugaji kuwa walinzi wa miti ambayo imekuwa ikipwandwa kwa ajili ya utunzaji wa mazingira,huku akitaka jamii kuwa walinzi na kuitunza miti ambayo itakwua inapandwa katika maeneo mbalimbali.


No comments:

Post a Comment