Thursday, March 22, 2012


WAFANYAKAZI MBALIMBALI WA MUSWA WAKIPANDA MITI.

AFISA MAHUSIANO WA MUWSA DORA KILO NAE AKIPANDA MTI KWENYE ZOEZI LA UPANDAJI WA MITI KWENYE CHANZO CHA MAJI CHA SHIRI.
MKURUGENZI WA MAMLAKA YA MAJI SAFI NA MAJI TAKA MUWSA ANTHONY KASONTA(KATIKATI)AKIFURAHIA ZOEZI HILO LA UPANDAJI MITI.

Imeelezwa kuwa endapo uharibifu wa mazingira ukiendelea kufanyika Mkoani Kilimanjaro kuna hatari ya ukame wa kuendelea kuongezeka,tofauti na hali ilivyo sasa ambayo imechangia kukauka kwa vyanzo vya maji na mabadiliko hewa yanayosababisha kuwepo kwa joto kali.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi maji na maji taka Mjini Moshi(MUWSA)Anthony Kasonta wakati wa zoezi la upandaji miti kwenye chanzo cha maji cha shiri kilichopo Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro.

Amesema kuwa  hali ya upatikanaji wa maji siyo nzuri licha ya kuwepo kwa mvua zilizonyesha hivi karibuni kutokana na ukame ambaoo  ulikuwa umesababishwa na uharibifu wa mazingira kwa kukata miti ovyo ambayo imesababisha kukaukwa kwa uoto wa asili na vyanzo vya maji.

Alisema kuwa zoezi hilo la kupanda miti kwenye vyanzo vya maji litakua endelevu,pamoja na kumuunga mkoni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama katika jitihada za kutunza mazingira kwa kupiga vita ukataji wa miti na kupanda miti.

Akizungumzia suala la uhaba wa maji lililosababishwa na ukame hivyo kuwepo kwa mgao wa maji kwa manispaa ya Moshi,hali ya upatikanaji wa maji bado haijarudi katika hali ya kawaida licha ya mvua zilizonyesha siku za hivi karibuni hivyo kusema bado mgao huo unaendlelea ila hauna makali kama ilivyokuwa awali.

Jumla ya miti 600 ilipandwa katika chanzo hicho cha maji ambayo itatunzwa na mamlaka hiyo,huku akisema kuwa mwanzo wa maji katika vyanzo vilivyopo mbali kama mlima Kilimanjaro hivyo wananchi wanatakiwa  kutunza mazingira bila kujali kwamba kuna chanzo cha maji au hamna.


Kasonta alisema kuwa suala la uharibifu wa mazingira ndilo lilipolekea kuwepo kwa mgao wa maji ambao ni mara ya kwaza mgao wa maji kuwepo Mjini hapa,huku akisema mazingira yasipotunzwa kizazi kinachokuja kinaweza kukosa kabisa maji pamoja na miti.



No comments:

Post a Comment