Sunday, April 28, 2013


.
 Timu ya waandishi wa habari ya mpira wa pete(waliovalia jezi za rangi ya njano)wakiwa na wachezajiw a Marenga Investment.

 Katika mtanange huo timu ya Waandishi wa habari iliweza kuibuka kidedea kwa kuwafunga Marenga mabao 35 kwa mabao 12 hadi mwisho wa pambano.



        KWA UPANDE WA MPIRA WA MIGUU MAMBO NAYO YALIKUWA HIVI
           WAANDISHI WA HABARI 5-MARENGA 3 HADI DAKIKA 90.
Mchezo huo wa kirafiki ulirushwa moja kwa moja na radio moshi fm ambapo waandishi wa habari walianza kupata bao lao la kwanza dakika ya 1 ambapo hadi kipindi cha kwanza kinamalizika waandishi waliokuwa wakiongoza kwa bao 3.

Hadi mwisho wa mpira waandishi waliongoza timu zote za mpira wa miguu na mpira wa pete hivyo kuweka historia mpya katika uwanja wa mpira wa Chuo Kikuu cha Ushirika(MUCOBS) Mjini Moshi.

 Hapa ni timu ya waandishi wa habari wakingozwa na james Paul wa kwanza kushoto wakijiandaa kuingia uwanjani wakiwa wamevalia jezi nyekundu kama za Man United.
 Timu ya Marenga wauza unga hawa waliweza kulambishwa unga na Sukari hatimaye kumwaga chozi uwanjani.


No comments:

Post a Comment