ADHARI NA SABABU ZA KUSHUKA KWA KILIMO CHA KAHAWA KIUCHUMI.
Wadau mbalimbali,kulia Venance Mallel akiangalia moja ya miche ya kwanza kupandwa na Missionary Mkoani Kilimanjaro. |
Mche wa kahawa ambao una miaka mingi. |
Vicky
Swai (40) mkazi wa kijiji cha Mbeera Kata ya Machame Uroki Wilayani Hai ambaye
ni mjane na mama wa watoto watano kwa muda mrefu alitegemea kilimo cha
kahawa,lakini baada ya kushuka kwa uzalishaji
kumeathiri kwa kiwango kikubwa maendeleo yake kiuchumi.
Wakati
wa uhai wa mume wake ambaye amefariki mwaka 2004 walikuwa wakivuna hadi kilo 900
kwenye shamba la hekta 2 ambapo waliuza na kupata kipato
kilichowatosha kutumia mpaka kipindi cha kuvuna tena kahawa.
Anasema
kuwa hali ya maisha kwa sasa ni tofauti kwani amelazimika kuwa mfanyabisha mdogo(machinga)baada ya kilimo hicho kukosa
muelekeo.
Vicky
anasema kuwa kilichomkatisha tamaa ya kutoendelea na kulima zao hilo ni pamoja na kutumia
garama kubwa kwenye uzalishaji lakini kuuza kwa bei ya chini.
Anasema
kuwa kilimo cha kahawa kwa miaka ya 1998 walikuwa wakilima na kupata hadi tani
1000 kwa hekta mbili walizokuwa wakilima, ,tofauti na miaka ya 2000 kuendelea
ambayo wamekuwa wakipata tani 200 kwenye hekta hizo.
“Mimi mume wangu alikuwa akilima zao la Kahawa
na alikuwa akipata magunia mengi,na hata baada ya kufariki mwaka 2004 kahawa
tulizokuwa tunazitegema zilianza kutoa kahawa kidogo,huku zikishambuliwa na
wadudu hatimaye kushindwa kuzihudumia kutokana na kuhitaji garama
kubwa”Alisema.
Hata
hivyo kupitia kilimo hicho anasema kuwa waliweza kuwasomesha watoto,kujenga na
majukumu mengine,lakini maisha anayoshi kwa sasa ni yatofauti kidogo baada ya
kufa kwa zao la kahawa.
Kilimo
cha zao la kahawa kinategemewa na wananchi kwenye Wilaya zaidi ya nne zilizopo Mkoani
hapa,ambazo ni Wilaya ya Hai,Siha, Moshi, na Rombo,ambzao maendeleo yao
yanategemea kilimo cha kahawa.
Katika
kushuka kwa uzalishaji wa zao la Kahawa hakujamuadhiri Vicky peke yake bali
wapo wakulima wengine ambao nao wameamua kujitafutia shughuli nyingine,baada ya
kujiondoa kwenye kilimo cha kahawa.
Bashiri
Andrew (45)ambaye ameamua kuikata mibuni ya kahawa na kulima mazao ya muda
mfupi aina ya nyanya,yeye anasema kuwa mazao aliyolima yamekuwa na soko la
uhakika,pamoja na kutochukua garama kama ilivyo kahawa.
Bashiri
anasema kuwa Serikali imejitoa katika kuwahudumia wakulima wa kahawa
pembejeo,tofauti na ilivyokuwa ikifanya kipindi cha nyuma,hivyo kuchangia pia
wakulima wengi kukata tamaa.
“Mimi
nilikuwa mkulima mzuri wa kilimo cha kahawa lakini ikafika wakati kilimo hicho
kikawa ni hasara kwetu,kutokana na kupanda kwa garama za uzalishaji,huku bei
ikishuka kwenye soko la dunia”Alisema Andrew.
Anasema
kuwa wananchi wamekuwa wakilima zao hilo kila mwaka huku mafanikio yakiwa ni
madogo kutokana na pembejeo za kilimo kuuzwa ghali,na upatikanaji wa miche kuwa
wa shida na gharama kubwa.
Alex
Munuo (50) mkazi Wilayani Rombo yeye
anasema kuwa maisha ambayo walikuwa wakiishi kwa kutegemea kilimo cha
kahawa na ilivyo sasa ni tofauti,kutokana na kilimo hicho kuwa kama uti wa
mgongo wa uchumi wa familia.
Anasema
kuwa mafaniko waliyonayo ikiwemo nyumba wanayoishi walijenga kwa kilimo
hicho,kuanzisha miradi mbalimbali pamoja nakuwapia watoto elimu na mahitaji
mengine ya familia.
Uzalishaji
wa zao la kahawa ulikuwa umejigawa katika makundi mbalimbali ikiwemo mashamba
ya wawekezaji,yale ya vyama vya ushirika,pamoja mashamba ya watu binafsi.
Hali
ya kilimo cha kahawa kukosa muelekeo
anasema kuwa imesababisha wanachi wengi kuyatelekeza mashamba yao,na
kuamua kujiingiza kwenye biashara nyingine ili kuweza kumudu maisha yao.
Miongoni
mwa changamoto ambayo ilionekana kuwa kubwa na kuelezwa na kila mkulima kwenye
Wilaya za Hai,Siha,Rombo na Moshi wakulima wengi walieleza kukatishwa tamaa
kukosekana kwa soko la uhakiki,pamoja na bei ndogo.
Wakulima
wanasema kuwa ilifika wakati kahawa ikashuka bei kutoka shs. 1500 kwa kilo
mwaka 1997/98 hadi shs. 500 kwa kilo mwaka 2002/03, wakati gharama ya
uzalishaji kilo moja ya kahawa ikiwa shs. 800 mpaka 1200,hapo kukapelekea
wakulima wengi kuacha kabisa kulima kahawa
Madhara ya
kushuka kwa uzalishaji wa zao la Kahawa Mkoani Kilimanjaro.
Wakulima
ambao walikua wakilima zao hilo la kahawa wanasema kuwa baada ya uzalishaji wa
kahawa kushuka,wazazi wengi walishindwa kuwasomesha watoto shule pamoja na
vijana wengi kuamua kujiingiza kwenye biashara ndondogo maarufu kama machinga
na kupanda mlima kama wabeba mzigo.
“Zao
la kahawa lilisaidia kwa kiasi kikubwa kwenye maendeleo ya familia
walizokuwa wanalima zao hilo kwani wakati wa uzalishaji ulivyokuwa mzuri
maisha yao yalikuwa mazuri,tofauti na yalivyo sasa uzalishai uliposhuka”Alisema
Hamisi Juma mmoja wa wakulima.
Gift
Matious ni miongoni mwa mwananchi,mkazi Mwika Wilaya ya Moshi Vijijini ambaye
anasema kusuasua kwa uzalishaji wa zalo hilo kumekuwa na madhara kwa wananchi wa Mkoa wa Kilimanajaro kwa ujumla.
Anakumbushia
kipindi cha nyuma wakati uzalishaji wa kahawa ukiwa mzuri,pia kulikuwepo na
huduma muhimu ambazo zilikuwa zikitolewa kwa jamii kupitia vyama vyake vya
ushirika,ambavyo vilikuwa vikiundwa na wakulima wa zao hilo.
Anasema
vyama vya ushirika vilikuwa na maduka ya ushirika ambayo yalikuwa yakiuza
bidhaa mbalimbali,kwa wananchi,na wakati mwingine kupatiwa huduma hata
kama hawana fedha taslimu na kulipa kwa
kukatwa kwenye malipo wanapouza kahawa.
Pia
vyama hivyo vilikuwa vikitoa pembejeo za kilimo kwa wakulima,hali ambayo baada
ya kusitishwa kwa pembejeo kumewafanya wananchi wengi kushindwa kununua
pembejeo hizo kutokana na kuuzwa gali.
“Baada ya kufa kwa uzalishaji wa zao la kahawa
kuna baadhi maeneo vyama vya ushirika navyo vimekufa,majengo yake
yamebomoka,hivyo wananchi hawapati huduma iliyokuwa ikitolewa na ushirika
pamoja na wengine kupoteza ajira”Alisema Mongi.
Katika
uuzwaji wa kahawa kwa vyama vikuu pia kulikuwapo na fedha za akiba ambazo
alikuwa akilipwa kila mkulima mara baada ya kuuza kahawa kulingana na bei
ambayo ingeuzwa kwenye soko la dunia.
“Wakati
wa uzalishaji wa zao la kahawa ukiwa mzuri Umoja wa wakulima wa zao hilo kupitia
chama Kikuu cha ushirika pia waliweza kuwa na miradi kama mahoteli,Benki,ambazo
zilikuwa zikitoa huduma ,hivyo zao hilo lingekuwa linaendelea vizuri huenda
wangekuwa na miradi mingi zaidi kama mashule na hata Vyuo vya elimu ya
juu.”Alisema Mongi
Mwenyekiti
wa KNCU Mynard Swai anakiri kufa kwa baadhi ya maduka hayo ya ushirika ambayo
anasema pia yalikuwa yakiuza vifaa mbalimbali,ikiwemo vya ujenzi na zana za
kilimo.
Hivyo
anasema kuwa kushindwa kufanya kazi kwa maduka hayo kutokana na madhara ya kushuka
kwa uzalishaji kumechangia wananchi kukosa huduma muhimu.
“Maduka ya ushirika
yalikuwa hayaendeshwi kibiashara kwa lengo la kupata faida kubwa,yalikuwepo kwa
ajili ya kutoa huduma kwa wakulima,hivyo yaliweza kuuza vifaa mbalimbali
ikiwemo vya ujenzi na kusaidia wakulima wengi kuwa na nyumba bora”Alisema.
Kwa
upende wake Mkurugenzi wa Manispaa ya moshi Bernadette Kinabo anasema kuwa
kushuka kwa uzalishaji wa kahawa,kumechangia kwa kiasi kikubwa kufa kwa viwanda
vya Moshi.
Anasema
viwanda vilikuwa vinategemea kutoa huduma kwa kuwepo kwa mahitaji kwa wakazi wa
mkoa wa Kilimanajaro,lakini baada ya kushuka kwa zao wa kahawa,kulipelekea
viwanda zaidi ya 15 kushindwa kufanya kazi.
Mbali
na viwanda kufa,lakini pia anasema hali ya kufa kwa zao hilo kumechangia kuwepo
kwa wimbi kubwa la wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga ambao walikuwa
wakitegemea kilimo pamoja na kufanya kazi kwenye mashamba ya wakulima.
Mbali
na kufa kwa viwanda lakini uchumi wa wakazi wengi wa moshi akamaanisha kipato
cha wananchi kimepungua,huku wengine wakiwa hawana kazi,pamoja na kushindwa
kuchangia kazi mbalimbali za maendeleo.
“Kilimo
cha kahawa kilikuwa muhimu kwa wananchi Mkoani hapa,na baada ya zao hili kukosa
muelekeo basi hata maendeleo ya wananchi na Mkoa yamekuwa nyuma,ndio maana
Serikali inafanya juhudi mbalimbali kufufuza zao la kahawa”Alisema Kinabo.
Sababu za kushuka
kwa uzalishaji
Wakulima
wengi kwenye Wilaya Hai,Siha,Rombo na Moshi Vijijini ambao mwandishi wa makala
hii aliweza kuzungumza nao walieleza kuwa sababu ambazo zimepelekea kushuka kwa
zao hilo kuwa ni pamoja na kushuka kwa bei,na kupanda kwa garama za uzalishaji.
Pia
wanasema kuwa Serikali kutotoa ruzuku ya pemebejeo kwa wakulima,licha ya kuwepo
kwa garama kubwa za uzalishaji nako kukachangia wakulima wengi kukata tamaa
kabisa ya uzalisha na kuamua kulima mazao mengine.
Mwenyekiti
wa chama kikuu cha ushirika Mkoani Kilimanjaro,(KNCU) Mynard Swai anakiri
kushuka kwa uzalishaji wa zao hilo,na kusema kuna sababu mbalimbali
zilizopelekea kushuka kwa uzalishaji.
Anasema
kuwa kilimo hicho kilipanda miaka ya 1997/98 kwa Mkoa wa Kilimanjaro kuweza
kuzalisha hadi tani 11325 lakini
ulishuka tena kwenye miaka ya 2007/8 na kufika tani 3495,kutokana na changamoto
mbalimbali.
Miongoni
mwa changamoto iliyopeleka uzalishaji kushuka ni pamoja na Mibuni mingi ya zao
la kahawa inayotunzwa na zaidi ya asilimia 60 inamiaka zaidi ya 40.
Mibuni
kuwa na umri mkubwa inasababisha uzalishajikushuka kwa mkulima kupata kilo 200 badala ya zaidi ya kilo 500 kwa
hekta zinazoweza kuzalishwa katika shamba lenye mibuni mipya.
Sababu
nyingine ya kushuka kwa uzalishaji ni pamoja na
mashambulizi ya magonjwa ya chulebuni (CBD) na kutu ya majani (CLR)
kusababisha hasara kubwa ya mazao toka shambani pamoja na kuharibu ubora wake.
“Pembejeo
za kilimo kama madawa zimekuwa zikipatikana kwa garama kubwa,hivyo mkulima
kushindwa kumudu garama hizo,hususani ni pale mibuni inapokuwa inashambuliwa na
magonjwa kutokana na hali ya hewa”Alisema Swai.
Huduma
duni za ugani na ukosefu wa vitendea kazi hasa vyombo vya usafiri kwa Maafisa
Ugani pamoja na ukosefu wa mafunzo ya mara kwa mara na uhaba wa
wataalamu pamoja na kupungua kwa maeneo ya kulima kahawa kutokana na
maeneo hayo kutumika katika ujenzi wa makazi ya watu.
Hali ya uzalishaji kwa sasa
Mkurugenzi
Mkuu wa bodi ya Kahawa,injinia Adolph
Kumburu akizungumza na mwandishi wa makala hii kuhusiana na uzalishaji wa
kahawa kwa
kipindi cha miaka 5 anasema uzalisjaji
umekuwa wa wastani wa tani 50,000 za kahawa safi ambayo imekuwa ikizalishwa
nchini.
Uzalishaji
huo kwa kipindi cha miaka mitano nchini
umekuwa wa kupanda na kushuka, kutokana na msimu na hali ya hewa,ambapo
mwaka jana 2011/12 uzalishaji ulishuka hadi tani 33,000 za kahawa safi toka
tani 54,000 mwaka 2010/11.
Anasema kuwa kwa mwaka huu 2012/2013
uzalishaji huo unatarajiwa kupanda na kufikia tani 55,000 angalau kuweza
kufikia uzalishaji wa mwaka 2010/2011 ambao uzalishaji wake wa kahawa ulikuwa
tani 54,000 kwa Tanzania nzima.
Anasema
kuwa Mkoa wa Kilimanjaro,kwa sasa unazalisha kiasi cha tani 4,000 tu za kahawa
safi ambayo ni sawa na asilimia 8 tu ya kahawa yote nchini.
Hapa
ndipo uzalishaji wa zao la kahawa unajidhirisha kushuka,kutokana na ukweli
kuwa kipindi cha nyuma kwenye miaka ya
1997 Mkoa wa Kilimanjaro pekee ulikuwa ukizalisha zaidi ya asilimia 30-36 ya
kahawa yoye iliyokuwa ikizalishwa nchini.
“Kwa
kipindi cha miaka mitano uzalishaji wa zao la kahawa kama hali ikiwa nzuri kwa
Mkoa wa Kilimanjaro umekuwa ukichezea kwenye kati ya tani 3,000 hadi 9,000
kulingana na hali ya hewa”Alisema Kumburu.
Soko la Kahawa
likoje?.
Kahawa inayozalishwa nchini
inategemea zaidi soko la nje,kutokana na asilimia 95 ya kahawainayozalishwa
nchini kuuzwa nje ya nchi na asilimia 5
ndiyo inayouzwa kwenye soko la ndani.
Kutokana
na hali hiyo ni dhahiri kuwa bei itakuwa inategemea zaidi soko la dunia na aina
ya kahawa,mbaya zaidi ni pale nchi ambazo zinanunua kahawa kwa wingi
zinapokumbwa na mdororo wa uchumi,wakulima wa kahawa huwa na kilio zaidi.
Adolph
Kumburu anasema kahawa huuzwa nje ya nchi ikiwa safi (clean) na ikiwa katika
madaraja,huku masoko ya kahawa aina ya Arabika yakiwa Marekani na kahawa za
Robusta yakiwa Uingereza.
Bei
ya Kahawa kwenye soko la dunia kwa msimu huu wastani wa bei kwa kahawa za
Arabica ni shilingi 5000 za kitanzania na kwa kahawa za robusta ni shilingi
3200.
Kuhusu
upatikanaji wa soko la uhakika,Kumburu anasema kuwa zao hilo kwa sasa lina soko
la uhakika na siyo kama kipindi cha nyuma,ila cha kuzingatia ni kuzalisha
kahawa yenye ubora ili kupata bei nzuri.
Jitihada za
kuimarisha Kilimo cha Kahawa.
Kutokana
na soko la kahawa kutegemea zaidi masoko nje ya nchi, kama Japan, Ujerumani,
Marekani, Uholanzi, Italia na Ubelgiji,jitihada mbalimbali zinahitajika
kuimarisha soko letu la ndani ili kutotegemea kwa kiasi kikubwa kupangiwa bei
na soko la dunia.
Kumburu
anasema kuwa zipo jitihada mbalimbali ambazo zinafanywa na bodi hiyo ya kahawa
katika kuhakikisha soko la ndani linakuwa zaidi ya asilimia 5 iliyopo kwa sasa.
Miongoni
mwa mikakati ni pamoja na Kuhamasisha wananchi kunywa kahawa yao na kupata
manufaa ya kunywa kahawa kiafya licha ya kupata kiburudisho tu,na wakati
mwingine kuitumia kama tiba ya kiafya.
Pia
kufanywa kwa uhamasishaji katika taasisi za serikali na katika maonyesho mbali
mbali kama vile nanenane na sabasaba kuhusu unywaji wa kahawa,ikiambatana na
faida za kunywa kahawa.
Lakini
pia zipo jitihada mbalimbali ambazo zinafanywa na uongozi wa Mkoa wa
Kilimanjaro,kutokana na umuhimu wa zao la kahawa kwa uchumi wa mkoa,kwa
kushirikiana na chama kikuu cha Uhsirika Mkoani Kilimanjaro(KNCU).
Miongini mwa jitihada hizo ni pamoja na taasisi ya
Serikali ya utafiti wa kahawa(TaCri)kwa
kushirikisha vikundi vya wakulima kuanzisha bustani za miche kwenye maeneo yao
wakulima ili kurahisisha upatinaji wa miche bora ya kahawa,
Kujenga
na kufufua viwanda vya kumenya kahawa (central pulperies)ambavyo vilikuwa
vimekufa, baadhi ya vikundi/watu binafsi kuruhusiwa kuuza kahawa yao ya ubora
wa juu moja kwa moja nje na kupata bei nzuri
Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika Mnard Swai
anasema kuwa chama hicho kwa kushirikiana na taasisi ya utafiti ya zao la
kahawa,(Tacri)wameweza kusambaza miche mipya zaidi ya 500,000 kwa wakulima wa
kahawa miche ambayo ni ya kisasa.
Pia anasema kuwa chama hicho kumewaajiri maafisa
ugani,hivyo kusaidia kuongeza idadi ya maafisa ugani kutoka 8 hadi 29 ambao
wamekuwa wakifanya kazi kwa ukaribu na wakulima na kugaramiwa vifaa vya kazi na
KNCU.
Anasema lengo ni kuongeza tija katika uzalishaji
kutoka kilo 200 kwa hekta hadi kilo 600-1000 kwa kupanda aina bora za kahawa
zilizozaliswa na TACRI ambazo zinauwezo wa kuzuia magonjwa pamoja na kuwa na
uzalishaji mzuri.
“Kilimo cha kahawa kinategemea bei kutoka nje ya nchi
na ndio wanapanga bei ya zao hilo,hivyo KNCU kwa kushirikiana na wadau wa
kahawa tunajiahidi kuhakikisha kuwa kahawa inayozalishwa inauzwa asilimia 40
nchini”Alisema Swai.
Tanzania
inazalisha kahawa namba 1 (clear)kwa wastani wa tani 50,000 na hii ni sawa na
asilimia 0.8 ya uzalishaji wote wa dunia.
Miongoni
mwa Mikoa inayoongoza katika uzalishaji ni pamoja na Kagera ambao uzalisha wake ni asilimia 30 hadi 40% ya kahawa yote
inayozalishwa Nchini.
Kwa
upande wa pato la taifa kahawa huchangia asilimia 15 ya sehemu ya kilimo
(agricultural GDP)ambapo jumla ya mchango wa sekta ya Kilimo kwenye pato la
taifa ni asilimia 24.7 .
No comments:
Post a Comment