WANANCHI WANAOZUNGUKA MLIMA KILIMANJARO WATAKIWA KUUTUNZA MLIMA HUO KWA KUFANYA USAFI.
Wananchi wanaoishi katika Vijiji vinavyouzunguka milima
Kilimanjaro, wametakiwa kujijengea tabia ya kufanya usafi ndani na nje ya mlima huo, kwa lengo la
kuokoa Ikolojia ambayo imeonekana kuuadhiri kwa kiasi kikubwa hususani kwenye
vyanzo vya maji.
Wito huo ulitolewa jana na Kaimu katibu Tawala mkoa
wa Kilimanjaro Gadison Lengwana wakati
wa kuzindua kampeni ya kufanya usafi ndani ya mlima huo, ambapo jumla ya watu
90 walipanda kwaajili ya zoezi hilo.
Lengwana alisemaa kuwa uchafu mwingi umekuwa
ukichangiwa na wapagazi na waongoza watalii, kutokana na wao kutupa taka ngumu
kandokando ya barabara na kuziacha, hali inayochangia uhariifu mkubwa wa
mazingira.
Alisema kuwa kutokana na taka hizo zinaweza kuhatarisha Ikolojia ya mlimaa,
vyanzo vya maji, pamoja na kupunguza idadi
ya wagenia endapo hatua za hara hazitachukuliwa kwa mamlaka husika pamoja na
jamii iliyoko karibu na hifadhi ya mlima huo.
Lengwana alisema kuwa elimu inahitajika zaidi kwa
watanzania hususani wanaopanda juu ya
umuhimu wa kusafisha na kuhifadhi misitu ya asilihi kwa kupanda miti mingi kwa lengo la kuendeleza
Ikolojia yam lima huo.
Kwa upande wake mhifadhi mkuu wa Mlima Kilimanjaro
KINAPA, Erastos Kufungulo, alisema kuwa lengo la kushirikisha jumuia zote
zinazouzunguka mlima kuona umuhimu wa kuifadhi na kuboresha mazingira.
Alisema kuwa kampeni hiyo imeshirikisha wafanyakazi
wa hifadhi ya mlima huo na baadhi ya wananchi, ambapo watapanda wakifanya usafi
hadi kileleni kwa siku kumi wakipitia
njia tatu za Machame, Marangu na Mweka.
Mwisho
No comments:
Post a Comment