Friday, March 9, 2012


Taarifa zilizotua hivi punde kupitia mwanahabari wa mtandao huu wa www.tanzania-leo. blogspot.com kutoka chumba cha habari za radio Uhuru zinadai kuwa Rais Jakaya Kikwete amesogeza mbele hotuba yake kwa Taifa aliyopanga kuitoa leo majira ya saa 10 jioni kupitia wazee wa mkoa wa Dar es Salaam katika ukumbi wa Diamond Jubilee na sasa Rais Kikwete atalihotubia Taifa jumamosi majira ya saa 5.00 asubuhi katika ukumbi huo.

Inadaiwa rais amefanya hivyo ili kupisha mazungumzo zaidi baada ya mahakama ya kazi kusitisha mgomo wa madaktari .

Tuwe pamoja kuendelea kupata hotuba hiyo...


No comments:

Post a Comment